Na Judith Mhina – MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli, anahitaji kupata usaidizi wa kutosha kutoka kwa
viongozi na hasa wasaidizi kuanzia ngazi
ya nyumba kumi hadi taifa.
Maneno hayo yametamkwa na Waziri Mkuu
mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba alipofanya mahojiano na Idara ya Habari –
MAELEZO - ofisini kwake Oysterbay Jijini Dar-es-Salaam.
Jaji Warioba ameona kuna udhaifu
mkubwa wa kiutendaji ambapo wananchi hawatoi changamoto zinazowakabili mpaka
wamuone Rais amefika katika eneo lao, au wanaeleza changamoto zinazowakabili kwa
viongozi husika ila, viongozi hawazifanyii kazi, ambapo wananchi wanaamua
kuziwasilisha kwa Rais mara wanapomuona.
“Rais hawezi kufanya kazi peke yake naomba
tuimarishe utendaji wetu wa kazi, kama utendaji ungekuwa mzuri suala la makontena
kufika hadi bandarini lisingekuwepo, na hata kugundulika kwake kusingefanywa na
Rais,” amesema Jaji Warioba.
“Nampongeza sana Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kwa utendaji wao wa kazi.
Viongozi hawa ni wasikivu na wanatekeleza kazi zao bila mihemko kwa kutoa
maagizo na maelekezo kwa wahusika ili wayatekeleze”, aliongeza Mhe. Warioba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...