Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
KUELEKEA
uchaguzi Mkuu wa Chama cha Soka la Wanawake unaotarajiwa kufanyika
Jumamosi ya Julai 08 wagombea wa nafasi mbalimbali wameanza kujinadi
sera zao wakiahidi kuendeleza vyema soka la wanawake linaloanza kushika
kasi kwa sasa.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti, wagombea hao wanaotetea nafasi zao wamesema kuwa
wanatarajiwa kuendeleza pale walipoishia katika awamu waliyotoka kwani
wanaamini kuwa wakirejea katika nafasi zao maendeleo ya soka la wanawake
yatazidi kukua.
Mwenyekiti
anayetetea nafasi yake, Amina Kaluma amesema kuwa atahakikisha
anazidisha mahusiano mazuri na mashirikisho mengine ya soka kutoka nchi
tofauti ikiwemo kujitangaza zaidi kwenye soka la wanawake.
Amina
amesema kuwa, atatumia nafasi yake kama Mwenyekiti kuwashawishi wakina
mama kuwaruhusu watoto wao kucheza mpira wa miguu ikiwemo kuwahamasisha
wao kama wanawake kusaidia katika kuinua soka la wanawake kwani asilimia
kubwa nao ni mashabiki wa mpira.
"Nitatumia
nafasi yangu kuwahamasisha wakina mama kujiwekeza zaidi katika soka la
wanawake kwani asilimia kubwa wao ni mashabiki na pia waweze kuwaruhusu
watoto wao wa kike kucheza mpira wa miguu kwani
hauna uhuni kama wengi wanavyosema,"amesema Amina.
Kwa
upande wa Mgombe wa nafasi ya Katibu Mkuu anayetetea nafasi yake Somoe
Ng'itu amesema kuwa katika kipindi chao cha miaka minne iliyopita
wameweza kuhakikisha ligi ya wanawake inachezwa na ikiwa katika ubora wa
hali ya juu pamoja na kupata udhamini.
Mbali
ba hilo wameweza kushiriki katika Kombe la Afrika Mashariki na Kati na
kufanikiwa kutwaa ubingwa huo kwa mara ya kwanza, TWFA imeweza kuwa na
timu za vijana za Taifa kwa upande wa wanawake kwa umri wa miaka 17 na
20 huku kwa mara ya kwanza ikijumuisha wachezaji kutoka nchi nzima.
Uchaguzi wa wanawake utafanyika Jumamosi huku kampeni za Uchaguzi zikiwa zimeanza Julai 4 mwaka huu.
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Chama cha soka la Wanawake Amina Kaluma akinadi sera zake mbele ya wanahabari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...