Mkazi wa kijiji cha Mwande kata ya Mateteleka halmashauri ya wilaya ya Madaba,mkoani Ruvuma Thobias Ngulungula akitoa malalamiko yake ya ahadi ya Rais Dkt John Magufuri ya kutoa shilingi milioni 50 kwa kijiji mbele ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba Shafi Mpenda(hayupo pichani)wakati wa mkutano wa hadhara kijijini hapo jana. ambapo ameiomba serikali kuharakisha ukutekeleza ahadi hiyo ili iwasaidie wananchi kuanzisha vikundi vya kiuchumi katika vijiji vyao.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma Shafi Mpenda akizungumza jana na wakazi wa kijiji cha Mwande kataya Mateteleka wilayani Songea katika mkutano wa hadhara uliolenga kuhamasisha kazi za maendeleo kijijini hapo baada ya serikali kuanzisha kijiji hicho kwa lengo la kusogeza huduma mbalimbali za kijamii karibu na wananchi wa kijiji hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...