Benny Mwaipaja, WFM-Dar es Salaam
Zikiwa zimebaki siku tatu kati ya siku 15 zilizoongezwa na Serikali kwa wananchi kulipa kodi ya majengo bila adhabu, baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wameiomba Serikali iongeze muda mwingine zaidi ili watu wote waweze kulipa kodi hiyo bila adhabu kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa zoezi hilo.
Wananchi hao wamemweleza Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alipofanya ziara za kushitukiza katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA-Mtaa wa Kipata-eneo la Mnazi Mmoja na Mbagala mkoani Dar es Salaam
Wamesema kuwa mwamko wa wananchi kulipa kodi ni mkubwa hali iliyosababisha foleni kubwa kila mahali nchini kutokana na uhaba wa watumishi wa TRA pamoja na vitendeakazi muhimu kama vile kompyuta na mashine za kielektroniki za kutolea risiti (EFDs).
Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango amewataka Watanzania kuwa watulivu na kuendelea kulipa kodi hiyo huku akiahidi kutatua changamoto ya uhaba wa watumishi pamoja na vitendeakazi ili kuwaondolea adha wananchi waliojitokeza kwa moyo kulipa kodi mbalimbali ikiwemo ya majengo.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akiongea na wananchi waliojitokeza kulipa kodi ya majengo katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)-Ilala Mtaa wa Kipata, na kuwapongeza kwa kuitikia wito huo kwa wingi na kuwaeleza kuwa kwa kulipa kodi kutasaidia upatikanaji wa huduma muhimu kama maji, barabara, umeme  na dawa hospitalini.
 Wananchi waliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ilala Mtaa wa Kipata, wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kulia) akiwaelezea namna atakavyoboresha huduma kwa walipa kodi za majengo kwa kuwapa kipaumbele walemavu, wazee, wagonjwa na wasiojiweza. Tukio hili litaenda sambamba na kuwawekea sehemu maalumu ya kukaa wakati wakisubiri huduma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) akipokea shukrani na pongezi kutoka kwa Bi. Rose Muyalo, kwa utendaji makini wa Serikali ya Awamu ya Tano na kwa kupatiwa huduma bora kutoka kwa wafanyakazi wa TRA.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kulia) akiongea na wananchi waliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ilala Mtaa wa Kipata kulipa kodi za majengo na kuelezea furaha yake namna walivyoitikia wito huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...