Na Sixmund J. Begashe wa
Makumbusho ya Taifa
Watanzania wameshauriwa kuunga mkono jitihada mbali mbali
zinazofanywa na Serikali, Mashirika ya Umma na Wadau mbali mbali katika mapambano
dhidi ya rushwa ili kutokomeza kabisa
tatizo hili hapa nchini.
Hayo
yamesema na Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam Bwana Achiles Bufure kwenye usahili uliofanywa
na Makumbusho hiyo ili kuchaguwa wasanii watakao unda kikundi kimoja kwa lengo
la kutoa elimu ya Mapambano dhidi ya Rushwa hapa nchini.
Wakizungumza
baada ya Usahili huo, msanii Bi Yame Muhamedi wa Kikundi cha sanaa cha UKOO na
Salum Mbaya wa St Kamilius Wameipongeza Makumbusho ya Taifa kwa kuwashirikisha
wasanii katika program ya MUSEUM ART EXPLOSION AGAINST CORRUPTION kwani imewapa nguvu na hari ya kuendelea kufanya
kazi za sanaa katika kuleta matokeo chanya ya kimaendeleo ndani ya nchi na
kuahidi kufanya vyema kazi iliyopo mbele yao ya kufikisha ujumbe kwa jamii juu
ya madhara ya Rushwa nchini.
Program
ya MUSEUM ART EXPLOSION AGAINST COTTUPTION ni moja kati ya program tano nchini
zilizopata ufadhili wa Ubalozi wa Uswiss wenye lengo la kutoa elimu kwa
watanzania juu ya Madhara na namna ya kupambana na Rushwa nchini.
Wasanii kutoka vikundi mbali mbali wakifanya
usajili kabla ya usahili.
Wasani wakiwajibika katika
usahili uliofanyika Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam ili kupata
nafasi ya kushiriki mapambano dhidi ya rushwa kupitia sanaa.
Usaili ukiendelea jukwaani
Kushoto ni Mkurugenzi
wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw. Achiles Bufure akifuatilia kwa karibu zoezi la usahili
kwa wasanii lililofanywa na Makumbusho
hiyo. Kulia ni Msanii Nguli wa sanaa za Jukwaani Bw Aloyce Makonde akitoa
maelezo kwa wasanii wakati wa usahili huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...