Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) amesema Watumishi wa  Umma walioghushi vyeti watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Mhe. Kairuki alisema hayo katika kikao kazi na watumishi na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke,Tarafa ya Mbagala mapema leo.
Mhe. Kairuki alisisitiza kuwa wote  walioghushi vyeti hawapo kazini na wameshafutwa katika orodha ya malipo ya Serikali (payroll) na kuelekeza waajiri kuwafuta wote wasiostahili kuwepo katika orodha ya malipo na wasimsubiri hadi afike katika maeneo ya kazi ili kutekekeza hilo.
“Baada ya zoezi la uhakiki kukamilika, hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa walioghushi vyeti kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na miongozo iliyopo katika Utumishi wa Umma” Kairuki alisema.
Aidha, aliwataka waajiri kuhakikisha wanahakiki taarifa za watumishi wapya wanapoajiriwa na wale wanaohamia ili kujiridhisha kama wana vyeti safi.
“Ni wajibu wa kila Mwajiri kuhakikisha kuwa Vyeti vya kila mwajiriwa mpya vinathibitishwa na Mamlaka husika kabla ya kumwajiri na hatimaye kumuingiza kwenye Orodha za Malipo ya Mishahara (Payroll) kupitia kwenye Mfumo wa HCMIS na Mifumo mingine ya mishahara ya kitaasisi.”
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah J. Kairuki akizungumza na viongozi na watumishi wa umma wa tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke alipofanya ziara katika tarafa hiyo kwa ajili ya kusikiliza kero za watumishi wa umma leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Tawala Wilaya ya Temeke Bw. Hashim Komba
 Afisa Elimu Kata ya Mbagala Kuu Bibi. Mindi Kuchilingulo akichangia mada wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah J. Kairuki kusikiliza kero za watumishi wa umma leo katika tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam.
 Katibu Tawala Wilaya ya Temeke Bw. Hashim Komba akifafanua jambo wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah J. Kairuki kusikiliza kero za watumishi wa umma leo katika tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mhe. Waziri Angellah Kairuki
 Mkurugenzi Idara ya Utawala wa Utumishi wa Umma Bw. Issa Ng’imba akielezea shughuli zinazofanywa na idara yake wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah J. Kairuki kusikiliza kero za watumishi wa umma leo katika tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watumishi wa umma kutoka tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke wakifuatilia hoja zilizokua zikiendelea wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Angellah J. Kairuki kusikiliza kero za watumishi wa umma leo katika tarafa ya Mbagala Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam. Picha na Genofeva Matemu - Maelezo. 
                                                      Taarifa kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...