Na Karama Kenyunko-Globu ya jamii.
RAIA wa Uganda, Edwin Gusongoirye (30) na Mfanyabiashara, Steven Simon (45) wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka ya uhujumu uchumi kwa kuisababishia serikali hasara ya Sh milioni 210.2.
Gusongoirye ambaye ni mfamasia pamoja na Simoni wamesomewa mashitaka yao sita mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa.
Hati ya mashitaka hayo, imsomwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga na kudai kuwa kati ya Machi 6 na Juni 22, mwaka huu jijini Dar es Salaam, washitakiwa walitengeneza mfumo wa kutumia huduma za mtandao kwa lengo la kukwepa kodi ya kupokea na kusambaza mawasiliano bila kuwa na kibali kutoka TCRA
Imedaiwa kuwa kati ya Machi 6 na Juni 22, 2016, washitakiwa hao kwa pamoja waliendesha mfumo wa kupokea na kusambaza mawasiliano ya Kimataifa bila kuwa na leseni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Katika shtaka la tatu kuwa, imedaiwa kuwa, Gusongoirye na Simon waliingiza vifaa vya mawasiliano nchini ambavyo ni maboksi matatu ya simu bila kuwa na kibali cha TCRA.
Aidha, washtakiwa hao wanadaiwa, kabla ya Machi, 2012 jijini Dar es Salaam, walisimika vifaa mbalimbali vya mawasiliano zikiwemo kompyuta mpakato mbili aina ya Dell na Hp bila kibali.
RAIA wa Uganda, Edwin Gusongoirye (30) na Mfanyabiashara, Steven Simon (45) wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka ya uhujumu uchumi kwa kuisababishia serikali hasara ya Sh milioni 210.2.
Gusongoirye ambaye ni mfamasia pamoja na Simoni wamesomewa mashitaka yao sita mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa.
Hati ya mashitaka hayo, imsomwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga na kudai kuwa kati ya Machi 6 na Juni 22, mwaka huu jijini Dar es Salaam, washitakiwa walitengeneza mfumo wa kutumia huduma za mtandao kwa lengo la kukwepa kodi ya kupokea na kusambaza mawasiliano bila kuwa na kibali kutoka TCRA
Imedaiwa kuwa kati ya Machi 6 na Juni 22, 2016, washitakiwa hao kwa pamoja waliendesha mfumo wa kupokea na kusambaza mawasiliano ya Kimataifa bila kuwa na leseni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Katika shtaka la tatu kuwa, imedaiwa kuwa, Gusongoirye na Simon waliingiza vifaa vya mawasiliano nchini ambavyo ni maboksi matatu ya simu bila kuwa na kibali cha TCRA.
Aidha, washtakiwa hao wanadaiwa, kabla ya Machi, 2012 jijini Dar es Salaam, walisimika vifaa mbalimbali vya mawasiliano zikiwemo kompyuta mpakato mbili aina ya Dell na Hp bila kibali.
Watuhumiwa, Steven Simon, aliyetangulia mbele na Edwin Gusongoirye, raia wa Uganda, wakipelekwa mahakamani kusomewa kesi yao ya uhujumu uchumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...