Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akitoa hotuba yake mbele ya maafisa wa Magereza pamoja na watendaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, katika Ukumbi wa Magereza Karanga, Mjini Kilimanjaro Mkoani Kilimanjaro, Julai 14, 2017. Waziri Mhagama alifanya ziara ya kutembelea na kukagua eneo la Mradi wa Ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za ngozi cha karanga kilichopo mkoni Kilimanjaro ambacho kipo chini ya Mfuko wa Pesheni wa PPF kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini. Kiwanda hicho kilikuwa kinazalisha viatu 150 kwa siku na sasa kinatarajiwa kufikia viatu 400 baada ya kukamilika kwa ukarabati.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mgwira, Katibu mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji, Prof. Adof Mkenda pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt, Juma Malewa wakiangalia sehemu ya Bidhaa za Ngozi zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu cha Magereza Karanga, Mkoani Kilimanjaro, Julai 14, 2017. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akichukuliwa kipimo cha mguu kwa ajili ya kutengenezewa Viatu vinavyotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu cha Magereza Karanga, Mkoani Kilimanjaro, Julai 14, 2017. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakiangalia moja ya mashine za kutengeneza viatu, katika Kiwanda cha Viatu cha Magereza Karanga, Mkoani Kilimanjaro, Julai 14, 2017. Wengine ni Kamishna wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, Hassan Bakari Mkwiche pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio akitoa taarifa fupi ya uwekezaji uliofanywa na mfuko huo kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza katika ukarabati wa kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Magereza Karanga kilichopo Mkoni Kilimanjaro.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...