Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisalimiana na watumishi wa kitupo cha afya cha mji mdogo wa Katoro, mkoani Geita.Waziri huyo amefika katika  kituo hicho ili kujionea hali ya kituo hicho ambacho kinahudumia idadi kubwa ya wakazi wa mji huo pamoja na jirani zake licha ya kuwa na changamoto ya watumishi pamoja na miundombinu.
 Waziri Ummy akimsalimia mtoto aliyefika kituoni hapo pamoja na mama yake kupata huduma ya afya,kulia ni Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho Dkt. Peter Janga
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akimfafanulia jambo mmoja wa wagonjwa waliofika kupata huduma kwenye kituo cha afya cha Katoro
 Waziri Ummy akitoa maelekezo kwenye matangazo yaliyobandikwa kwenye kuta za kituo hicho,kushoto ni Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA Geita Lawrence Kalabezile.Waziri huyo amewataka watumishi wa kituo hicho kujituma na kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wananchi hususan katika kuokoa maisha ya wagonjwa.
Katika ziara hivyo Waziri Ummy alikagua ujenzi wa jengo la upasuaji wa dharura unaojengwa kwenye kituo hicho.Waziri wa Afya yupo  katika ziara ya kikazi ya  siku tatu Mkoani Geita (PICHA ZOTE NA WIZARA YA AFYA)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...