Waziri wa Fedha na Mipango Mhe Dkt. Philip Isdor  Mpango  (Mb)  akiongea na mmoja wa wananchi (anayemuonesha karatasi ) waliofika kulipa kodi ya majengo katika ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) – Kigamboni, ambapo alieleza kuridhishwa na utendaji wa watumishi katika mamlaka hiyo.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), aliyevaa miwani na kukunja mikono, akiwa amejichanganya katika kundi la wakazi wa mji wa Kigamboni waliojitokeza kulipa kodi ya majengo katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania-Kigamboni, akiwa na lengo la kuchunguza namna wananchi wanavyopata huduma. 

 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe Dkt. Philip Isdor Mpango  (Mb) (kulia) akisalimiana na mmoja wa wakazi wa Mji wa Kigamboni waliojitokeza kulipa kodi katika Ofisi za mamlaka ya mapato Tanzania TRA-Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe Dkt. Philip Isdor  Mpango  (Mb), akiwapongeza na kuwashukuru wananchi wa Kigamboni waliojitokeza kulipa kodi ya majengo na kutoa rai kwa wananchi kujenga utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari ili kufikia uchumi wa viwanda na kuendesha huduma za jamii.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiamuru Kituo cha Mafuta cha Mjimwema Kigamboni kifungwe, baada ya kubaini kuwa wamiliki wamekiuka masharti kwa kutotumia mashine maalumu za kielektroniki ya kutolea risiti hatua inayoikosesha Serikali mapato ya kodi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...