Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Amina Salum anaratajiwa kuwa mgeni rasimi kesho katika ufungaji wa maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara nchini (Tantrade) ilisema kuwa maonesho hayo yataitimishwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Amina Salum ambaye atatoa vyeti kwa washindi wa mabanda bora yaliyoshiriki maonesho hayo.

Taarifa hiyo ilisema kuwa maonesho hayo yatafungwa majira ya saa saba kwa hotoba ya Waziri huyo na kufuatana na viongozi mbalimbali wakiwemo waandaji wa Maonesho hayo.

Wakati huo katika maonesho hayo wananchi wameendelea kufika katika viwanja vya sabasaba kwa kupata huduma pamoja bidhaa za washiriki.

Mabanda ambayo yamekuwa na watu katika siku ya maonesho tangu siku kwanza hadi leo ni mabanda Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pamoja na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Katibu Mkuu wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji , Profesa Adolf Mkenda akimpa maelekezo Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) ,Mcharo Mrutu katika maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji , Profesa Adolf Mkenda akisaini kitabu cha wageni katika maonesho ya 41 ya biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...