Katibu mkuu (mwenye koti nyeusi) akikata utepe wa uzinduzi wa ofisi ya pori la piti kulia kwake ni kaimu mkurugenzi mkuu wa tawa bw.martin loibooki na kushoto nimeneja wa pori la rukwa/piti bw.ambrose mungo’ng’o .

Na Mwandishi wetu Songwe

Taasisi ya Kimataifa ya kijamii ya uhifadhi wa wanyamapori ya World Concervation Society- WCS imetoa msaada wa zaidi ya shilingi milioni 936 kwa mapori ya akiba ya Lukwati- Piti ambazo zimetumika kujenga jengo la kisasa la ofisi, ununuzi wa magari matatu ya doria na kuendesha mafunzo ya askari wa wanyamapori wa mapori hayo yaliyoko mkoani Songwe.

Akiongea katika halfa ya kukabidhi miradi hiyo kwa serikali ya Tanzania, Mkurugenzi wa WCS Aaron Nicholaus amesema taaisisi hiyo inajivunia kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuendeleza shughuli za uhifadhi wa wanayamapori wakiwemo tembo ambao ni maliasili muhimu kitaifa na kimataifa ambapo shirika la misaada la watu wa Marekani USAID nalo ni mdau mkubwa katika ufadhili huo.
katibu mkuu akipokea magari 3 aina ya toyota l/cruiser pickup toka kwa mratibu wa mradi wa cws bw. Aaron nicholaus.

Bwana Nicholaus alisema msaada huo umetilia mkazo suala la mafuzo ambayo yatawaongezea askari ujuzi na weledi wa kukabiliana na majangili ambao wamekuwa wakiua tembo na wanyamapori wengine kwa maslahi yao binafsi na kusababisha hasara kwa serikali ambayo inawategemea wanyamapori kwa maendeleo ya jamii na taifa.

“Tunapofikiria uhifadhi, tuangalie pia masuala ya mapito ya wanyamapori kama tembo ambayo yamekuwa yakitoweka kutokana na kuongezeka kwa shughuli za binadamu na hivyo kuathiri uhifadhi maana tembo huhitaji eneo kubwa kwa malisho” alisme abwana Nicholaus.

Taarifa ya miradi hiyo iliyotolewa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudance Milanzi ilieleza kuwa miradi hiyo ina thamani kubwa kwa uhifadhi wa mapori hayo yenye ukubwa wa zaidi ya kilomita za mraba 6,119 ambayo yanapakana na Hifadhi ya taifa ya Ruaha na pori la akiba la Rungwa.
Katibu mkuu akiongea na baadhi ya kikosi cha askari waliyopata mafunzo ya kukabiliana na ujangili. 

Meneja wa Mapori ya Lukwati Piti Bwana Alphonce Ambroce Mung’ong’o akitoa ufafanuzo na mchanganuo wa gharama za miradi hiyo alisema jengo la kisasa la ofisi limegharimu zaidi ya shilingi milioni 227, magari matatu kwaajili ya doria yana thamni ya dola 255,000 za kimarekani boti na mfumo wa radio call una thamani ya zaidi ya shilingi milioni 234.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...