UONGOZI wa Klabu ya Yanga umejaza nafasi zilizoachwa wazi kwa mujibu wa katiba ibara ya 28:(1)d  ikiwa ni maazimio ya kikao cha Kamati ya Utendaji kilichokaa tarehe 15/7/2017.

Kikao hicho cha Kamati ya Utendaji kikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti Clement Sanga kimeweza kufikia maazimio hayo kutokana na ibara hiyo anakuwa na mamlaka ya kujaza nafasi zile zilizoachwa wazi na wajumbe wa kamati.

Kikao hicho kimeweza kuwateua wajumbe watatu ambao ni Mohamed Nyenge, Tonny Mark na Majid Suleiman ambao wataanza majukumu yao yataanza moja kwa moja wakichukua nafasi za wajumbe wawili walioamua kujiweka pembeni pamoja na  mjumbe aliekuwa mwenyekiti wa kamati ya mashindano Mhandisi Malume aliekwenda nje ya nchi kwaajili ya masomo.

Pamoja na hilo, uongozi wa Yanga mapema wiki hii iliweza kukutana na kufanya kikao na wachezaji wa zamani wa timu hiyo na kufikia maazimio mbalimbali yenye malengo ya kuisaidia timu yao na kushirikiana nao bega kwa bega.
Maazimio hayo ni :

1.Kuwashirikisha katika masuala ya klabu na kuwaweka karibu na klabu.

2.Kujenga umoja wa wana Yanga kwa ujumla.

3.Kuunda safu ya uongozi wao itakayorahisisha mawasiliano baina yao na uongozi wa klabu.

4.Kuweka kumbu kumbu kwaajili ya historia ya klabu na vizazi vijavyo kupitia wao.

5.Kusaidiana katika suala zima la ugunduzi wa vipaji vya wachezaji kwa manufaa ya klabu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...