Mkurugenzi
wa Masoko, Utafitii na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Tully
Mwambapa (wa pili kulia) akikabidhi funguo ya gari mpya aina ya Toyota
Land Cruser kwa aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni
aliyehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi hilo Kitengo cha Mafao na Fidia, SACP Suzan Kaganda (wa nne
kushoto) ikiwa ni makabidhiano ya gari la kusaidia doria kwa Kituo cha
Polisi Kawe, Jijini Dar es salaam. Gari hilo lenye thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 70, limetolewa na Benki ya CRDB kwa kituo hicho. Hafla
ya makabidhiano hayo imefanyika mchana wa leo katika Kituo cha Kawe
jijini Dar es salaam. Wengine pichani kutoka kulia ni Kamanda wa Polisi
wa Kinondoni wa sasa, ACP Murilo Jumanne Murilo, Afisa Mtendaji Kata ya
Kawe, Husna Nond, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, OCD Jackson Simba
pamoja na Mkuu wa Kituo cha Polisi Kawe, ASP Samson Mwambungu.
Mkurugenzi
wa Masoko, Utafitii na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Tully
Mwambapa akizungumza katika hafla ya kukabidhi gari kwa Jeshi la Polisi
Kituo cha Kawe, jijini Dar es salaam.
Kamanda
wa zamani wa Polisi Mkoa wa Kinondoni aliyehamishiwa Makao Makuu ya
Jeshi hilo Kitengo cha Mafao na Fidia, SACP Suzan Kaganda akizungumza katika hafla ya kukabidhi gari kwa Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, jijini Dar es salaam.
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB PLC, Godwin Semunyu akiongoza hafla hiyo.
Meza kuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...