Pichani ni dereva wa gari la mwendokasi la DARTS  namba za usajili T.124 DGW akihojiwa baada ya kufanya kosa la kupita taa nyekundu eneo la Kibo barabara ya Morogoro jijini Dar es salaam leo asubuhi wakati akitokea Kimara kuelekea Kivukoni. Baada ya kukamatwa  hatua za kufikishwa mahakamani zinaendelea.
Mkuu wa usalama barabarani kanda maalum yaDar es salaam ACP Awadhi Haji  amesema baada ya kumkamata dereva huyo kwamba baadhi ya madereva wa magari hayo wamekuwa wakifanya makosa ya usalama barabarani mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kupita taa nyekundu, kutosimama kwenye vivuko vya waenda kwa miguu na kadhalika wakidhani kuwa wao hawawezi kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
"Hivyo naelekeza kuwa madereva hao wakamatwe na kuchukuliwa hatua kali kama madereva wengine pindi wanapobainika kuvunja sheria za barabani" ameamuru ACP Awadhi Haji ambaye huwa hana masikhara awapo kazini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...