NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
NAIBU Waziri wa Nishati na Madini,
Dkt. Medard Kalemani,(pichani anayeongea), amelitaka Shirika la Umeme
Tanzania TANESCO kuunganisha nguvu ili kuhakikisha wanakamilisha mradi
wa ujenzi wa kituo cha kupoza na kusamabaza umeme kinachotarajiwa
kujengwa huko Kimbiji wilayani Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Dkt.
Kalemani ametoa maelekezo hayo leo Agosti 22, 2017, wakati alipofanya
ziara kukagua miradi ya umeme kwenye kituo cha kupoza na kusambaza umeme
cha Kurasini, Kigamboni na eneo panapotarajiwa kujengwa kituo kingine
cha kupoza na kusambaza umeme huko Kimbiji wilayani Kigamboni jijini Dar
es Salaam.
“Hakikisheni mradi wa uejenzi wa kituo hiki cha
Kimbiji unakamilika ifikapo Machi 30, mwakani,(2018), na kuwaondolea
adha ya upatikanaji wa umeme wananchi wa Kigamboni, chukueni mafundi
waliokamilisha kazi ya kujenga kituo cha umeme kule Mtwara waje hapa,
muwaache wale wanaojenga transition (njia ya kusafirisha umeme) wajenge,
lakini wale mafundi wengine waleteni hapa ili mradi huu ukamilike.”
Alifafanua.
Akiwa kwenye kituo cha kupoza na kusamabza umeme
cha Kurasini jijini Dar es Salaam, Dkt. Kalemani aliipongeza TANESCO kwa
juhudi kubwa walizofanya kwa hatua ujenzi waliyofikia ambapo sasa
wameanza kufunga mashine kubwa. Kituo cha Kurasini ndicho
kinachotegemewa sana na watu wa Mbagala, Kurasini na Kigamboni.
Ongezeko
la haraka la wakazi kwenye maeneo ya Mbagala, na Kigamboni kumepelekea
uhitaji mkubwa wa umeme ambapo umeme unaopatikana kwa sasa umekuwa
haukidhi mahitaji ya wakazi wa maeneo hayo.
“Naomba niwaambie,
mradi huu umechelewa sana, hivyo basi ongezeni kasi ili ifikapo Agosti
30, mwaka huu, mradi ukamilike nataka watu wa Mbagala, watu wa Kurasini,
na watu wa Kigamboni wanaondokana na kero hii ya umeme, na mimi
nitawaambia washeshimiwa wabunge wa Kigamboni Mheshimiwa Ndungulile
(Dkt. Faustin Ndungulile) na Mheshimiwa Mangungu (Murtaza Magungu)
Mbunge wa Mbagala kuhusu habari hii ili wawaambie wananchi wa maeneo
haya wawe wavumilivu kwani mradi huu sasa utakamilika.” Alisema.
Dkt.
Kalemani pia aliwaagiza viongozi wa TANESCO, kuhakikisha wanakusanya
nguvu kwa maana ya vifaa kutoka ofisi zote za TANESCO mkoa wa Dar es
Salaam, ili kuhakikisha wananchi wote wa Kigamboni wanaofikia 350
waliolipia ada za kuunganishiwa umeme wawe wamepelekewe umeme ifikapo
mwisho wa mwezi huu wa Agosti.Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji
wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka, aliwaambia waandishi wa habari kuwa
maelekezo ya Mheshimiwa Naibu waziri yatafanyiwa kazi kwa haraka ili
kuhakikisha kero hiyo inaondoka.
Msaidizi
wa Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia miradi, Mhandisi Khalid
James,(kulia), akimpatia maelezo Naibu waziri wa Nishati na Madini, Dkt.
Medard Kalemani, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kituo
cha kupoza na kusambaza umeme Kurasin jijini Dar es Salaam.
Msaidizi
wa Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia miradi, Mhandisi Khalid
James,(kulia), akimpatia maelezo Naibu waziri wa Nishati na Madini, Dkt.
Medard Kalemani, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa kituo
cha kupoza na kusambaza umeme Kurasin jijini Dar es Salaam.
TUNATOA MIKOPO YA HARAKA YA € 15000 Hadi $ 72000 KIASI CHOCHOTE CHA UCHAGUZI WAKO NA 2-4
ReplyDeleteSAA YA HUDUMA YA MAFANIKIO YA KUFANIKIWA NA 2% VIWANGO VYA RIBA KWA BIASHARA
NA BINAFSI
MADHUMUNI SASA TUMIA NA UJUMBE WA BARUA KWA:
philipmorganloanservice00@gmail.com
JAZA NA URUDI
Jina:
Kiasi cha Mkopo:
Muda:
Jinsia:
Nchi:
Lengo:
Namba ya simu ya mkononi:
JIBU LAKO NI LAZIMA MARA MOJA