Mkuu
wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na Kaimu Kamanda wa
Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam (DCP) Lucas Mkondya, alipowasili nchini
akitokea nchini Rwanda kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kubadilishana uzoefu
pamoja na kujadiliana juu ya njia za kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka,
usafirishaji wa binadamu na biashara ya dawa za kulevya.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akisalimiana na baadhi ya maofisa
wa Jeshi hilo, waliofika kumpokea alipowasili kutoka nchini Rwanda alipokwenda
kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kubadilishana uzoefu pamoja na kujadiliana
juu ya njia za kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka, usafirishaji wa binadamu
na biashara ya dawa za kulevya.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
(IGP) Simon Sirro (watano kulia) na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Rwanda,
Emmanuel Gassana(wanne kulia), wakiwa katika picha ya na Maofisa wa Jeshi la
Polisi Nchini Rwanda, baada ya kumaliza kikao kazi. Picha na Jeshi la Polisi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...