Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kesi ya kutoa lugha chafu dhidi ya Rais John Pombe Magufuli inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee hadi Septemba 12, kwa kuwa hakimu anayesikiliza kesi hiyo anaudhuru.

Hata hivyo, kabla ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Mshtakiwa Mdee  kupitia mawakili wake amewasilisha pingamizi la awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwamba mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Mawakili wa Mdee, wakiongozwa na Hekima Mwesigwa wamewasilisha pingamizi hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa baada ya wakili wa serikali Leonard Chalo kudai shauri hilo limekuja kwa ajili ya kutajwa.

Mwesigwa amedai kuwa wanapingamizi mbili, kwanza hati ya mashtaka ina mapungufu, pia Mahakama hiyo haina mamlaka.

Amedai kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka kwa sababu, Mkuu wa wilaya aliyetoa amri ya kukamatwa kwa Mdee ameshindwa kufuata matakwa ya kisheria.

Hata hivyo, Hakimu Mwambapa hakujibu kitu chochote na ameiahirisha kesi     hiyo hadi September 12 mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...