Mpiga picha wa Globu ya Jamii mapema leo asubuhi amekumbana na adha ya usafiri,kufuatia Madereva katika kituo cha mabasi simu 2000 Manispaa ya Ubungo jijini Dar kugoma kutoa huduma ya usafiri,kwa kile walichodai kupandishiwa tozo kutoka shilingi 500 hadi 1000.

Akizungumza zaidi mmoja wa Madereva wa dala dala katika mgomo huo (hakutaka kujitambulisha jina),alisema kuwa wao hawawezi kulipa tozo hiyo wakati miundombinu ya kituo hicho si rafiki na hairidhishi kabisa kwa vyombo vyao vya usafiri.

"ni vyema wakazirekebisha kwanza changamoto kadhaa zilizopo hapa kituoni,kisha baadae waje na huo mkakati wao wa kutupandishia hiyo tozo yao,lakini kwa sasa itakuwa vigumu kulipa kwa sababu kama unavyoona mazingira yalivyo hapa kituoni",alisema mmoja wa Madereva.

Mpiga picha wa Globu ya Jamii pamoja na kuonja joto ya jiwe ya kukosa usafiri,pia alijionea adha waliokuwa wakiipata abiria wengine waliokuwepo kituoni hapo,huku baadhi ya abiria wakilazimika kutumia usafiri wa piki piki kuwahi kwenye shughuli zao na wengine wakitembea kwa Miguu. 

Mpaka Globu ya Jamii inaondoka kituoni hapo ufumbuzi bado ulikuwa haujapatikana.
 Madereva na Makondakta wakijadiliana kufuatia mgomo huo
Baadhi ya mabasi (dala dala) yakiwa yamepaki kituoni hapo yakisubiri mgomo huo upatiwe ufumbuzi.
 Baadhi ya abiria wakisubiri usafiri kituoni hapo mapema leo asubuhi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...