Na Bashir Yakub.
Mwanamke ameachwa na mume wake wa zamani. Lakini hajamuacha
kisheria. Hakumpa talaka isipokuwa waliachana tu kila mtu akaendelea na
maisha yake tena kwa muda sasa. Wewe umekutana na huyo mwanamke na
umeanzisha naye mahusiano. Umeanza kuishi naye au umeamua kabisa
kumuoa.
Ulimuuliza kuhusu mahusiano yake ya zamani akakueleza bila kukuficha
yaliyomsibu. Na wewe ukaona kwa kuwa tayari hayuko na huyo mume wake
wa zamani kwa muda mrefu au muda kiasi basi haina shida. Kitu cha
msingi kwako ulichozingatia ni kuwa hawa watu hawako wote tena kwa
maana mahusiano yao waliyasitisha.
Je sheria inasemaje kuhusu hali hii. Je kukaa na mwanamke wa namna hiyo
kwa maana ya kuishi naye bila ndoa, au kuishi naye kwa ndoa au kuwa
naye katika mahusiano bila kuishi naye kumezungumziwaje na sheria. Je
uko salama. Je hakuna lolote linaweza kukutokea likakusababishia usumbufu,
gharama, na kurehani mustakabali wa maisha yako. Je nini ufanye ikiwa
umo katika hali kama hiyo.
Haya na mengine yataelezwa hapa chini. Sura ya 29 ya sheria ya ndoa ,
iliyorekebishwa mwaka 2010 itatupatia majawabu ya maswali haya.
1.NI WAKATI GANI NDOA HUHESABIKA IMEVUNJIKA.
Ndoa ni zao la sheria na kufa kwake hufa kisheria. Ndoa haivunjiki
isipokuwa taratibu za kisheria zimefuatwa. Ndoa inaweza kuvunjika kwa kifo
cha mmoja wana ndoa, kwa kupotea kwa mda mrefu na kuihisiwa kufa kwa
mmoja wa wanandoa( presumption of death), lakini pia ndoa hufa/huvunjika
kwa talaka.
Kama mojawapo ya hayo juu halijajitokeza ndoa hiyo bado inaishi. Kwahiyo
mwanaume unatakiwa kujua kuwa mwanamke uliyemuoa au unayeishi nae
bila ndoa au uliye naye tu katika mahusiano ya kawaida , ikiwa hapo awali
alikuwa katika ndoa na mojawapo ya yaliyotajwa hapa juu hayajatokea basi
mwanamke huyo ndoa yake bado inaendelea. Hapo badae itaelezwa hatari
kubwa zinazokukabali .
2. JE KUTENGANA NI TALAKA.
Unaweza kudhani kuwa uko salama kwasababu una uhakika mwanamke
uliyenaye ametengana na mme wake wa mwanzo na hivyo wewe uko
salama. Kisheria kuna tofauti ya kutengana na kuachana/kutalikiana.
Kutengana sio talaka. Talaka ni talaka mpaka itolewe kwa mujibu wa sheria.
Pia kutelekeza sio kuachana/talaka. Watu wanaokuwa wametengana au
wametelekezana bila talaka fahamu kuwa watu hao kisheria bado ni
wanandoa.
Je ni muda gani wanandoa wakitengana,kwa mujibu wa sheri hii itahesabika imevunjika?
ReplyDelete