Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametembelea banda la
Maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA na kufurahishwa na ufanisi
mkubwa katika kuunganisha mifumo ya Serikali yenye kulenga utoaji huduma bora na
kurahisisha shughuli ya Utambuzi kwa wananchi.
Mheshimiwa Makamu wa
Rais ametembelea Banda la NIDA akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya kilele
cha maonyesho ya sikukuu ya Wakulima Kitaifa maarufu Nanenane yaliyofanyika
viwanja vya Ngongo mkoani Lindi. Mhe. Samia aliambatana na viongozi mbalimbali
wa Kitaifa akiwemo Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Dr. Charles Tizeba.
Katika maonyesho hayo
NIDA ni miongoni mwa Taasisi zilizofanya vizuri na kupata ushindi katika
makundi 15 yaliyotangazwa.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye
Banda la maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwenye maonesho ya NaneNane viwanja vya Ngongo mjini Lindi leo. Makamu wa Rais
alipokelewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi. Rose Mdami
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea taarifa ya shughuli za Usajili
ambazo zimekuwa zikifanyika katika Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
wakati wa Maonyesho ya Nanenane kwenye Viwanja vya Ngongo mjini Lindi.
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi. Rose Mdami
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo juu ya mashine zinazotumika kusajili na kutolea vitambuslisho vya Taifa toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi. Rose Mdami
Watumishi wa NIDA wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya
kupata ushindi kwenye maonyesho ya Nanenane kwa mwaka 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...