Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza na wananchi wa Mbande, Kata ya Chamazi, Tarafa ya Mbagala, Wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam, wakati alipofanya ziara katika eneo hilo yenye lengo la kuimarisha ulinzi na usalama katika eneo hilo. Hata hivyo, Masauni aliamuru ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande ambao utajengwa kwa michango ya wananchi na Serikali uanze mara moja, na pia aliwataka wananchi kutoa taarifa kwa kuwafichua askari polisi wanaohisiwa kushirikiana na wahalifu katika eneo hilo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Mkazi wa Mbande, Mbagala, jijini Dar es Salaam, Muhidin Maftaa alipokua anamuuliza swali kuhusu hali ya ulinzi na usalama katika eneo hilo. Ambaye alifanya ziara katika eneo hilo yenye lengo la kuimarisha ulinzi na usalama, aliamuru ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande ambao utajengwa kwa michango ya wananchi na Serikali uanze mara moja, na pia aliwataka wananchi kutoa taarifa kwa kuwafichua askari polisi wanaohisiwa kushirikiana na wahalifu katika eneo hilo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Gilles Muroto,alipokuwa anajibu mswali mbalimbali ya wananchi wa Mtaa wa Magengeni Mbande, Mbagala, jijini Dar es Salaam. Masauni alifanya ziara katika eneo hilo yenye lengo la kuimarisha ulinzi na usalama na aliamuru ujenzi wa Kituo cha Polisi Mbande ambao utajengwa kwa michango ya wananchi na Serikali uanze mara moja, na pia aliwataka wananchi kutoa taarifa kwa kuwafichua askari polisi wanaohisiwa kushirikiana na wahalifu katika eneo hilo.

habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...