Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga ameagiza shughuli zote za upimaji wa ardhi kusimama kwa sasa mpaka watakapotoa kibali cha upimaji.

Mkuu Wilaya alitoa agizo katika mkutano na wananchi wa wilaya kuhusiana na mgogoro wa ardhi, ambapo vijiji vinne vinavyodaiwa kuvamia shamba la familia ya Rajwani mwenye asili ya kihindi lenye ukubwa wa ekari 2472.

Vijiji hivyo vinne ni Mwambaya,Lunzando,Mipeko na mlamleni vilivyopo kwenye Kata ya mipeko na Tambani.

Sanga amesema kuwa kwa sasa hakuna mtu kutoka Halmashauri wala maafisa mipango miji kupima ardhi mpaka awe na kibali kutoka wilayani na kuongeza kuwa Madiwani na Wenyeviti wa vitongoji kutoruhusu mtu kupima ardhi mpaka awaoneshe kibali kutoka wilayani.

Aidha amewataka wananchi wa vijiji hivyo kifanya kazi zao kwa Uhuru bila hofu yeyote kwani wilaya hiyo ipo salama."tumejipanga vizuri Mimi mwenyewe ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama na wahakikisheni mupo salama,msiache kwenda mashambani,msiache mazao shambani kavuneni mazao yenu hakina wakuwabigudhi.alisema Sanga.

Wakati huohuo ametoa wito kwa madereva wabodaboda wilayani humo wametakiwa kuvaa kofia ngumu pindi wanapoendesha pikipiki na kuacha kupakia watu wawili kwa pikipiki moja ‘Mishakaki’.

Naye Mbunge wa jimbo la mkuranga Abdalah Ulega amewatoa hofu wananchi hao kwa kuwa suala lao linashughulikiwa na wamempa notisi ya siku 90 ya kujieleza kuhusiana na eneo hilo.

Ulega aliwaahidi wananchi hao kuwachangia kiasi cha shilingi milioni moja kama sehemu ya mchango wake katika kusaidia kutatua tatizo hilo.
 .Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga akizungumza na wananchi wa vijiji vinne ambavyo vina mgogoro wa ardhi katika mkutano uliofanyika Mwanambaya .
 Mbunge wa jimbo la Mkuranga , Abdalah  Ulega akizungumza na wapiga kura wake juu ya mgogoro wa shamba lenye ekari 90 katika kijiji cha Mkuranga.
 .Sehemu ya wananchi wakimsikiza mkuu wa wilaya juu ya mgogoro unao wakabili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...