Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella (katikati), akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi baada ya kuzindua Klabu ya Biashara mjini Mwanza hivi karibuni. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein. NBC imezindua Klabu ya Biashara iliyopewa jina la ‘NBC B-Club’ katika miji ya Kahama na Mwanza kwa kuandaa semina kwa wafanyabishara wajasiriamali.   NBC B-Club itasaida  huduma zisizo za kifedha kupitia mafunzo maalumu kwa kushirikiana  na wadau mbalimbali kuhusu mbinu za uendeshaji wa biashara na kuwajengea uwezo katika kuziendesha kwa ufanisi hivyo kukuza biashara hizo. 
  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi akihutubia wakati sherehe za uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara jijini Mwanza hivi karibuni. Wengine kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, aliyekuwa mgeni rasmi na Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Filbert Mponzi.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella akihutubia wakati wa semina ya wafanyabiashara katika uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara ya NBC mjini Mwanza. Wengine kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassim Hussein, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi na Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Filbert Mponzi. 
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya mika 50 ya benki hiyo mjini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (katikati), akizungumza na ujumbe wa viongozi wa NBC waliofika ofisi kwake kumtembelea wakiongozwa na Dk. Kassim Hussein (kulia kwake) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theoblad Sabi (kushoto kwake). NBC ilizindua klabu za biashara katika miji ya Kahama na Mwanza pamoja na kusherehekea miaka 50 tokea ilipoanzishwa.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...