Video Courtesy of MCL

JUKWAA la wahariri Tanzania (TEF) limeondoa zuio la kutokutoa habari za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Mkonda jijini humo leo.
Akizungumza na waandishi wa habari  katika hoteli ya Holiday Inn jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga amesema kuwa  Mgogoro kati ya Jukwaa la wahariri wa habari na tasnia ya habari  na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam umefika mwisho na kwamba TEF sasa inaruhusu habari zake ziandikwe na   mgogoro ule uliokuwepo uwe yaliyopita si ndwele, tugange yajayo"
Tamko hilo la TEF limekuja baada ya Machi 22 mwaka huu kutoa tamko lao kwa vyombo vya habari  lililokuwa likisema "Zinalaani vikali vitendo vya Mkuu wa Mkoa katika kuvamia chombo cha habari cha Clouds Media akiwa ameambatana na Askari wenye silaha.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam na  kuondoa adhabu aliyopewa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Kulia ni Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.
Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba akizungumza na waandishi wa  habari jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa mkutano wa Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) na wanahabari. Wa pili kulia ni  Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania(TEF), Deodatus Balile  na mshisho kulia ni Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.
Katikati ni  Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la wahariri Tanzania(TEF), Deodatus Balile  akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kushoto ni  Mkurugenzi wa Vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.  Habari na picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...