Na Agness Francis, Globu, ya jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda  ameahidi kutoa  msaada  wa  Miguu ya bandia kwa walemavu wa miguu wasio na uwezo wa kununua Miguu hiyo.

Akizungumza  na Waandishi wa Habari leo  jijini Dar es Salaam, Makonda amesema kuwa anatoa fursa hiyo kwa walemavu  200 ambapo itakuwa ni awamu ya kwanza kuweza kufanikisha zoezi hilo.

Makonda amesema zoezi hilo litafanyika kwa  awamu kutokana na gharama. Amesema  gharama hizo ni changamoto kwa wananchi wake kwa walio makazini na hata wasio makazini na amewaomba watumie fursa hiyo kujitokeza katika zoezi hilo la upimaji  vipimo ili kufanikisha leongo

Amesema kuwa zoezi hilo  litafanyika kwa siku mbili kuanzia Agosti 14-15 mwaka huu katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa zilizopo Ilala Boma Jijini Dar Es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akionesha Miguu Bandia kwa Waandishi wa Habari wakati kaizungumza nao Ofisini kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...