Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna
Mstaafu Zelote Stephen amezionya halmashauri zote mkoani Rukwa
kuhakikisha wanazitumia vizuri manshine za EFD kwa kuongeza mapato
katika halmashauri zao.
Ametoa onyo hilo kwenye kikao
maalum cha kujibu hoja za ukaguzi wa hesabu za serikali kwa madiwani wa
Manispaa ya Sumbawanga katika kumalizia ziara yake maalum kwa
halmashauri zote mkoani humo kujua namna Halmashauri zilivyojipanga ili
hoja hizo zisijirudie miaka inayofuata.
Akiongea huku akionesha risiti
alizozikamata katika maeneo mbalimbali ya mauzo alisema kuwa serikali
inafanya kila liwezalo katika kuhakikisha inakusanya maopato lakini bado
kuna watumishi wanatafuta namna ya kuiskosesha serikali mapato hayo.
“katika kila sehemu za mauzo
lazima mashine hizi ziwepo na kuwepo sio mtindo huu (akionesha msururu
wa risiti zilizokatwa tayari kwa matumizi) hizi nimezikamata maeneo
anajua Mkurugenzi, asubuhi watu wanagawana, ndio mchezo uliopo, pamoja
na jitihada tunazofanya bado watu wanatafuta mbinu za kuiba, hii sio
kwamba nimeleta iwe mfano, hapana, nimezikamata na mfahamu kuwa mimi ni
mtaalamu wa kukamata,”Alisema.
RC Rukwa Mh. Zelote Stephen akiwaonesha waheshimiwa madiwani (hawapo pichani)risiti ambazo tayari zimeshakatwa kabla ya kutumiwa.
RC Rukwa akiwaonesha waheshimiwa madiwani (hawapo pichani) kitabu cha hoja za mthibiti na mkaguzi wa serikali kwa Manispaa ya Sumbawanga.
RC Rukwa akitoa ufafanuzi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...