Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Bodi wa Taasisi ya Tanzania Health Promotion Support (THPS) Dkt. Augustine Massawe akizungumza katika uzinduzi wa Mpango Mkakati wa kusaidia mifumo ya afya wa miaka mitano ambao utatekelezwa kati ya mwaka 2016- 2020. Tukio hilo lilifanyika jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
(Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Mpango
Mkakati wa kusaidia mifumo ya afya wa miaka mitano ambao utatekelezwa
kati ya mwaka 2016-2020 na Taasisi ya Tanzania Health Promotion Support
(THPS). Tukio hilo lilifanyika jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya (wa nne toka Kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Redempta Mbatia (wa tako kutoka kushoto) pamoja na wadau wa afya wakionyesha chapisho la Mpango Mkakati wa kwanza wa kusaidia mifumo ya afya wa Taasisi ya Tanzania Health Promotion Support (THPS) ambao utatekelezwa kati ya mwaka 2016-2020.
Taasisi isiyo ya kiserikali ya Tanzania Health Promotion Support
(THPS) inayosaidia Wizara za afya Tanzania Bara na Zanzibar kutoa kinga
ya Virusi vya Ukimwi (VVU), huduma, matibabu na msaada kwa kuimarisha
mifumo ya afya imezindua mpango mkakati wa kwanza wa miaka
mitano.
Akizungumza katika uzinduzi
huo wa mpango mkakati uliofanyika Jijini Dar es salaam leo. Mwanzilishi
na Mwenyekiti wa Bodi wa THPS, Dkt. Augustine Massawe alisema mpango
mkakati wa kwanza wa taasisi hiyo ambao utatekelezwa kati ya mwaka 2016
mpaka 2020 umelenga kusaidia juhudi za Wizara ya afya, Serikali za
mitaa, Washiriki wengine na Wadau kuhakikisha huduma bora za afya
zinazoshugulikia afya ya umma ikiwemo magonjwa yanayoambukizwa na
yasiyoambukizwa ili kuboresha matokeo ya afya kiujumla katika jamii.
Dkt.
Massawe alisema anatarajia mpango mkakati utazingatia mawazo kati ya
wadau muhimu wa THPS na kujenga uamuzi wa pamoja wenye matokeo mazuri.
“tunataka kugusa maisha ya Watanzania wengi kwa kuathiri ubora wa huduma
za afya na kujenga taifa huru la VVU/UKIMWI. Nina matumaini kuwa mpango
mkakati uliofikiriwa utakuwa kama chombo cha usimamizi wa taasisi
katika kuweka vipaumbele, kuzingatia nishati na rasilimali, kuimarisha
shughuli mbalimbali na kuhakikisha wafanyakazi na wadau wengine
wanafanya kazi kwa malengo.
Akizungumzia juu ya
uzinduzi wa mpango mkakati, Mkurugenzi Mtendaji wa THPS, Dkt. Redempta
Mbatia alielezea malengo ya taasisi kwa miaka ijayo ni kutazamia mbali
VVU/ UKIMWI na kushughulika na magonjwa mengine yenye vitisho katika
jamii, kulenga katika uhamasishaji wa rasilimali na kuchunguza
ushirikiano wa pamoja na sekta binafsi ili kuendelea kutoa huduma zake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...