Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
akizungumza na wajumbe wa TFF (hawapo pichani) baada ya kutangazwa na
kuapishwa kwa viongozi wapya wa TFF Mkoani Dodoma.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw. Wallace Karia akitoa
neno la shukrani kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF kumwezesha kushika nafasi
ya urais, wakati wa Mkutano Mkuu wa TFF uliofanyika katika Ukumbi wa St. Gasper
Mkoani Dodoma.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
(kulia) akiteta na Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.
Michael Wambura (kushoto) baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa TFF
uliofanyika jana katika ukumbi wa St. Gasper Mkoani Dodoma.
Na Genofeva Matemu - WHUSM
Uongozi mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) umetakiwa kufikia
Januari mwakani kuwajibika kama mashirika mengine ya mpira wa miguu duniani
yanavyowajibika kuchapisha taarifa ya mapato na matumizi kwenye magazeti ili
wananchi wapate fursa ya kufahamu namna fedha zinavyopatikana na jinsi
zinavyotumika katika kuboresha na kuendeleza usimamizi bora wa soka nchini.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.
Harrison Mwakyembe wakati wa kufunga Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) na katika ukumbi wa St. Gasper Mkoani Dodoma
Aidha Mhe. Mwakyembe amewapongeza viongozi wapya waliochaguliwa kuiongoza TFF
kwa muda wa miaka minne kwa kuwataka kufanya kazi kwa ushirikiano na kwa
pamoja katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku huku akiwapongeza washiriki
wote waliothubutu kuwania uongozi katika nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi
Mkuu wa TFF wa mwaka huu.
Kwa upande wake Rais mpya wa TFF Bw. Wallace Karia amewaahidi wapiga kuwa
wake kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu kwani nafasi aliyopewa na wajumbe hao
kwa kumuamini ni deni ambalo atalilipa kwa kuleta mafanikio makubwa katika
mchezo wa soka.
Bw. Karia amesema kuwa furaha waliyonayo viongozi wote waliochaguliwa kuiongoza
TFF kwa muda wa miaka minne iende kuwa furaha ya kazi kwa kufanya yale
watanzania wanatarajia kutoka kwao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...