Ndugu wana Northampton kwa mujibu wa taratibu na kanuni tulizojiwekea na matarajio yetu ya muda mrefu, Kwa niaba ya kamati ndogo ya maandalizi naitisha Mkutano Mkuu na wa Uchaguzi wa Viongozi Wapya wa Jumuiya yetu ya Watanzania wote waishio Northampton na maeneo ya Wellingborough, Kattering na Corby (NORTHAMPTONSHIRE)  utakaofanyika siku ya Jumamosi tarehe 19/08/2017 katika ukumbi wa Norfolk Terrace, Semilong, Northampton NN2 6HS - Kuanzia saa kumi kamili jioni (4pm) mpaka saa mbili usiku (8.00pm).


Kamati ya maandalizi  inaomba ushirikiano wenu ili Kuepuka kupoteza muda siku ya mkutano, Tunaomba kila mjumbe mwenye ajenda ya ziada yeyote ambayo angependa iwepo katika kikao chetu basi asisite kunipatia siku nne kabla ya mkutano kwa njia ya Barua Pepe kwenda; suleimansalum160@yahoo.com au kwa kupiga simu ya Mkononi nambari 07963549935.
Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa  Tanzania Diaspora Community/Association in the United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland Ndugu Abraham Sangiwa, ambaye atatoa ufafanuzi wa jinsi Jumuiya zetu hapa Northampton zitakavoshirikiana na Jumuiya hii kuu katika malengo muhimu yanayotugusa wote Kama Watanzania tunaoishi Ughaibuni ili kupata ufumbuzi wenye nguvu zaidi kwa ushirikiano wetu.



Tujitahidi kuzingatia muda siku hiyo.  
UMOJA NA NGUVU
Suleiman Salum
Mwenyekiti Jumuiya ya Watanzania Northampton

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...