BENKI ya NMB Tanzania imedhamini ujenzi wa duka la Nafasi Art litakalotumiwa na watoto kujifunza mambo mbalimbali ambayo yanahusu sanaa ili kukuza vipaji walivyonavyo vya sanaa ili watakapokua waweze kuvitumia kutengeneza kipato. 
Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa duka hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke alisema udhamini huo ni sehemu ya malengo ya benki kuhakikisha inatenga pesa ambazo zitatumika kusaidia jamii.

 "Benki yetu imekuwa ikitumia kitengo cha CSR kusaidia jamii kwa kutenga pesa kila mwaka ambazo zinatumika kusaidia jamii, tunaamini kuwa ujenzi huu utasaidia kuinua vipaji vya watoto ambao wanapenda sanaa ili wainue vipaji vyao," alisema Ineke. 
Naye Mkurugenzi wa Nafasi Art Space, Rebecca Correy aliishukuru NMB kwa uufadhili ambao wamewapa na kuwa banda hilo litawasaidia watoto wanaopenda sanaa kuonyesha vipaji vyao kwani kwa kipindi kirefu watoto wamekuwa wakikosa nafasi ya kushiriki kufanya kazi mbalimbali za sanaa lakini kwa sasa wataweza kuonyesha vipaji vyao. 

Kwa upande wa mgeni rasmi kwenye halfa hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu aliipongeza NAFASI Art Space kwa jitihada ambazo inazifanya za kukuza sanaa nchini na kuwa Serikali ya awamu ya tano itandelea kushirikiana nao.
Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu, Mwenyekiti wa Bodi ya Nafasi Art Space, Davie Kitururu, Mkurugenzi wa Nafasi Art Space, Rebecca Correy na Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen wakifungua banda la NAFASI ya Watoto.
Mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa banda la NAFASI ya watoto, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Joyce Hagu akikata utepe kufungua duka la kuhifadhia kumbukumbu la NAFASI Art Space. Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker akizungumza kuhusu udhamini wa NMB na jinsi ambavyo wamejipanga kutoa misaada kwa jamii zenye uhitaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...