Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dk. Mussa
Mgwatu (kulia)akimuonyesha mkandarasi wa kampuni inayojenga maegesho ya Lindi
Kitunda Mhandisi Evans Martin eneo la maegesho ya kivuko wakati alipokua
akikagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho hayo mjini Lindi.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dk. Mussa
Mgwatu (wa pili kulia) aliyenyoosha mkono, akimuonyeshea Meneja wa TEMESA Mkoa
wa Lindi Mhandisi Greyson Maleko (wa kwanza kulia) eneo patakapojengwa chumba cha kupumzikia abiria wakati wakisubiria kivuko
upande wa Kitunda. Dk. Mgwatu alikua Mkoani humo kukagua ujenzi wa maegesho ya
Lindi Kitunda.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dk. Mussa
Mgwatu akimsisitizia jambo Mkandarasi wa
kampuni inayojenga maegesho ya Lindi Kitunda Mhandisi Evans Martin (wa kwanza
kushoto) wakati alipokua akikagua maendeleo ya ujenzi wa maegesho hayo mkoani
Lindi, nyuma yake ni Meneja wa Wakala wa Majengo (TBA) Mkoa wa Lindi Mhandisi Hillary Msaki.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dk. Mussa
Mgwatu kushoto Akimsikiliza Mhandisi Athaniel Kishebuka wakati alipotembelea
banda la wakala huo katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika
viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi. Dk. Mgwatu yupo mjini Lindi kukagua maendeleo
ya ujenzi wa maegesho ya Lindi Kitunda unaoendelea. PICHA ZOTE
NA ALFRED MGWENO (TEMESA)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...