Dodoma: Ikiwa zimebaki siku mbili kufika kikomo cha Maonyesho ya Kilimo na Mifugo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga amewataka wadau wa misitu nchini kuzalisha kwa tija mazao na bidhaa za mazao ya misitu na nyuki ili kufikia uchumi wa kati.

Akizungumza na wadau hao jana mara baada ya kutembelea Banda la Maliasili na Utalii katika Uwanja vya Maonyesho ya Kilimo Nzuguni - Dodoma alisema serikali imekusudia kuhakikisha inawawezesha wajasiliamari kufungua viwanda vidogo vidogo vitakavyozalisha kwa tija mazao na bidhaa mbalimbali ili kufikia uchumi wa kati.

Odunga alisema katika Mkoa wa Dodoma kuna eneo lililotengwa kwa ajili ya viwanda na kuwataka wadau wa misitu na nyuki kujiunga kwenye vikundi ili serikali iweze kuwasaidia kufungua viwanda vitakavyowawezesha kuzalisha bidhaa zenye ubora.

" Nimetumia muda mwingi kwenye mabanda ya wadau wa sekta ya misitu na nyuki kwa kuwa katika sera zetu tunataka kuona jinsi gani wananchi wanaweza kutumia misitu kwa kuzingatia matumizi endelevu ikiwa ni kutekeleza sera ya misitu na wakati huo huo kutekeleza sera ya viwanda kwa kuzalisha viwanda vinavyotumia malighafi za misitu," alisema Odunga.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Chemba-Dodoma, Simon Odunga (katikati) akipewa maelezo ya bidhaa zilizotengenezwa na malighafi za misitu (vinyago) na mdau wa Wakala wa Huduma za Misitu kutoka kampuni ya Kasana Artist kutoka Kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam, Bi. Rukia Katembo (mwenye sweta) katika Banda la Maliasili na Utalii Kwenye maonyesho ya Nane Nane Kanda ya Kati yanayofanyika Katika uwanja wa Nzuguni Dodoma kuanzia tarehe 01/08 hadi 08/08/2017 na kutoa wito kwa wananchi kutembelea banda hilo ili kuweza kujionea faida mbalimbali za uhifadhi wa misitu hususan katika kumuinua mwananchi kutoka uchumi wa kawaida hadi wa kati. Wa Mwisho kushoto ni mdau mwingine Angel Msangi.

Mdau wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzaniakutoka kampuni ya Jem Herbarist kutoka Bukoba inayozalisha bidhaa zake kwa kutumi mti wa Mlonge na Mshana, Bi. Janerose Mtayoba (mama mwenye kofia) akiwaeleza wananchi (wanaosoma maelezo ya dawa) waliotembelea Maonyesho ya Kilimo/Mifugo na Sherehe za Nane Nane Kanda ya Kati Dodoma matumizi ya dawa anazozalisha, kulia ni Katibu wa Chama cha Waganga na Wakunga wa Jadi Tanzania, Tabibu Issah Mkombozi akisikiliza maelezo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...