Na Mwandishi Wetu - MAELEZO

Kufuatia wito wa Rais John Pombe Magufuli alioutoa hivi karibuni, hadi kufikia jana tarehe 01 Agosti, 2017 jumla ya wakimbizi 6,700 raia wa Burundi wameshajiorodhesha kurejea nchini mwao kwa hiari.

Kufuatia hatua hiyo, Mkutano wa pande tatu utakaojumuisha Serikali za Tanzania, Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) unatarajiwa kufanyika mwishoni wa mwezi huu kujadili namna ya kuwarejesha nchini mwao wakimbizi hao kwa kuzingatia sheria za kimataifa zinazohusu wakimbizi.
 Katika mahojiano na mwandishi wetu ofisi kwake jana, Mkurugenzi Idara ya Huduma za Wakimbizi katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bwana Harrison Mseke alieleza kuwa tangu kutolewa kwa wito huo, Wizara imekuwa ikiwamahasisha wakimbizi hao wa kujiorodhesha kwa hiari ili waweze kurejea nyumbani.

Akiwa katika ziara yake kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa, Rais Magufuli alitoa wito kuwataka wakimbizi raia wa Burundi kurejea nyumbani kwa hiari kwa kuwa hali ya usalama nchini mwao ni nzuri ambapo wakati akitoa wito huo tarehe 20 Julai, 2017 huko Ngara aliambatana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza ambaye nae aliwahakikishia wakimbizi hao kuwa hali ni shwari nchini Burundi. 

Kwa mujibu wa Bwana Mseke, hivi sasa kuna wakimbizi raia wa Burundi 276,692 kati ya wakimbizi 348,019 walioko nchini. Wengine ni  wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) 70,840, Wasomali 150, na wengine (mchanganyiko) 337. 

Alifafanua kuwa kati ya idadi hiyo ya wakimbizi raia wa Burundi 242,340 waliingia nchini baada ya mwezi Aprili, 2015 kufuatia machafuko ya kisiasa nchini humo.
Akizungumzia mwendo wa uingiaji wakimbizi kutoka Burundi, alieleza kuwa kwa sasa kasi imepungua kutoka wastani wa wakimbizi 1,000 kwa siku kati ya mwezi Agosti hadi Disemba, 2016 hadi wastani wa wakimbizi kumi kwa siku katika miezi ya hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...