Na Mathias Canal, Lindi

Pamoja na mazao mbalimbali yanayolimwa na wakulima nchini Tanzania lakini wametakiwa kujikita zaidi na kilimo cha mazao yanayostahimili ukame ikiwemo kuanzisha kilimo cha umwagiliaji hususani katika maeneo yaliyopo pembezoni mwa Bahari ya Hindi katika Mikoa ya Mtwara na Lindi.

Kufanya hivyo ni kutumia vizuri rasilimali za nchi ikiwemo maji na maeneo oevu katika kilimo chenye tija jambo ambalo linatoa fursa kwa wakulima wadogo kuwa na kipato kikubwa na kutafsiri ipasavyo kipato cha nchi na mtu mmoja mmoja.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa maendeleo ya mazao Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi idara kuu ya kilimo Ndg Twahir Nzallawahe alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndg Methew J. Mtigumwe mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Nanenane katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndg Methew J. Mtigumwe akisoma na kupata maelezo mbalimbali kuhusu ufanisi katika Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) mara baada ya kutembelea banda hilo wakati wa Maonesho ya Nanenane katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndg Methew J. Mtigumwe akisikiliza maelezo ya namna ya ufyatuaji matofali yanayotumika kujengea nyumba za NHC mara baada ya kutembelea banda hilo wakati wa Maonesho ya Nanenane katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Ndg Methew J. Mtigumwe (Kushoto) akisikiliz akwa makini maelezo kuhusu ufanyaji kazi katika banda la TAMISEMI mara baada ya kutembelea banda hilo wakati wa Maonesho ya Nanenane katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi. Mwingine ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi Mhe Rukia Muwango.
Mkurugenzi wa maendeleo ya mazao Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi idara kuu ya kilimo Ndg Twahir Nzallawahe akisikiliza maelezo mbalimbali katika banda la Nanyamba mara baada ya kutembelea banda hilo wakati wa Maonesho ya Nanenane katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...