Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Stewart Rory alipofika Wizarani tarehe 22 Agosti, 2017 kwa ajili ya mazungumzo rasmi na Waziri Mahiga. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Uingereza. Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lale la Kimataifa la Maendeleo (DFID) inaisadia Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Maji, Elimu, Nishati Mbadala na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya. Mhe. Stewart yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 22 na 23 Agosti, 2017. 
Sehemu ya ujumbe ulioambatana na Mhe. Stewart. Kulia ni Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Sarah Cooke, Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Uingereza (DFID), Bi. Beth Arthy na Afisa kutoka Ubalozini. 
Sehemu ya ujumbe wa Wizara wakati wa mazungumzo kati ya Waziri Mahiga na Waziri Stewart kutoka Uingereza (hawapo pichani). Kushoto ni Bw. Salvatory Mbilinyi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Bw. Joseph Kapinga, Afisa Mambo ya Nje.
Waziri Mahiga akiagana na mgeni wake Mhe. Stewart mara baada ya kumaliza mazungumzo yao .
Picha ya pamoja
Waziri Mahiga kwa pamoja na Mhe. Stewart wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu lengo la ziara ya Mhe. Stewart nchini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...