Lengo ni kufikia Watanzania wengi na waweze kuwa na kaunti za hundi kwa bei nafuu.
Dar es Salaam Tanzania, BancABC imeendelea kuwa Benki inayojiogeza hapa nchini kwa kua wabunifu wa hali ya juu kwenye utoaji huduma zao pamoja na kuboresha huduma hizo za kibenki ili kuwawezesha wateja kupata huduma za kwa urahisi na hivyo kuwa suluhisho kwenye sekta ya fedha.

Katika kuendelea kudhihirisha ubunifu wa bidhaa zao, BancABC leo imezindua akaunti mpya inayoitwa Jiongeze Hundi akaunti kwa lengo la kupunguza makato ya huduma za uendeshaji akaunti ya mwezi kwa mwezi kwa wateja wote watakaofungua Akaunti ya Jiongeze na Benki hiyo hapa nchini.

Akaunti ya Jiongeze inamfanya mteja aweze kuendesha akaunti ya kibiashara au ya mshahara mara nyingi bila makato ya mwisho wa mwezi kwa muda wa mwaka mmoja na hivyo kufanya wateja wa BancABC kuweza kufanya miamala mingi ya kibenki kwa Uhuru na urahisi zaidi.
 Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa akaunti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato yeyote ya mwisho wa mwezi. Kushoto ni Meneja Masoko wa benki hiyo Upendo Nkini.

Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) na  Meneja Masoko wa benki hiyo, Upendo Nkini, wakionyesha bango la   uzinduzi wa akauti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato ya mwisho wa mwezi wakati wa hafla ya kuzindua akaunti hiyo jijini Dar es Salaam jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...