Mkurugenzi
Mtendaji wa BANK OF AFRICA – TANZANIA, Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah
akizindua rasmi program ya SWAHIBA Mobile App. Kulia kwake ni mkuu wa
kitengo cha rasilimali watu wa benki hiyo Ms. Mercy Msuya na Meneja
Masoko, utafiti na maendeleo wa benki hiyo ndg. Muganyizi Bisheko.
BANK OF AFRICA – TANZANIA imezindua programu yake mpya ya kibenki inayoitwa "SWAHIBA Mobile" kwenye soko la Tanzania. Huduma hii inakuja kama muendelezo wa programu ya B- Mobile, inayoruhusu watumiaji kufurahia huduma kamili za kibenki kupitia aina yoyote ya simu za mkononi, wakati wowote.
BANK OF AFRICA – TANZANIA imezindua programu yake mpya ya kibenki inayoitwa "SWAHIBA Mobile" kwenye soko la Tanzania. Huduma hii inakuja kama muendelezo wa programu ya B- Mobile, inayoruhusu watumiaji kufurahia huduma kamili za kibenki kupitia aina yoyote ya simu za mkononi, wakati wowote.
SWAHIBA
Mobile App inawapa wateja urahisi wa kutumia huduma za kibenki katika
simu kwani inakuja na muonekano mzuri Zaidi na sifa nyingi mpya
zinanzowarahisishia wateja kufuatilia akaunti zao za binafsi na za
kibiashara kwa wakati mmoja.
Huduma
zipatikanazo kwenye programu hii ni: huduma za kuhamisha fedha, huduma
za hundi, maombi ya mkopo wa papo hapo, malipo ya bili mbalimbali,
huduma za utoaji fedha kwenye ATM bila kadi, kuongeza muda wa maongezi,
usajili binafsi wa mobile banking na huduma za e-chama pamoja na
nyingine nyingi.
Emmanuel Mshindo, Mkuu wakitengo cha Huduma mbadala za kibenki akitoa maelezo juu ya huduma mbalimbali zipatikanazo katika program ya SWAHIBA Mobile, wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma hiyo mapema hii leo.
Zaidi
ya hayo, SWAHIBA Mobile APP inaweza kutumiwa na Mtanzania yoyote hata
ambae si mteja wa BANK OF AFRICA. Hii ni kupitia huduma mbalimbali
zinazopatikana kabla ya kuingia kwenye program yaani “without Log in
services”. huduma hizi ni kama vile maelezo kuhusu Huduma mbalimbali
zitolewazo na BANK OF AFRICA, Maombi ya Mikopo, maelekezo kuhusu yalipo
Matawi ya BANK OF AFRICA na ATMs, pamoja na viwango vya ubadilishaji
fedha za kigeni.
Mr.
Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA -
TANZANIA alisema Benki yake inajivunia kuanzisha programu hii mpya ya
benki kiganjani katika wakati huu muhimu ambapo benki hiyo inaadhimisha
miaka 10 ya biashara katika nchi ya Tanzania. "Uzinduzi wa SWAHIBA
Mobile App ni namna ya kipekee ya kuwasilisha shukrani zetu kwa wateja,
jamii, washirika, wamiliki na wadau wote, walio tupa ushirikiano wa
kutosha katika kipindi cha miaka 10 ya kazi nchini ".
Naibu Mkurugenzi wa BANK OF AFRICA Bw. Wasia Mushi, akiongea na wageni waalikwa (hawapo pichani) katika hafla ya uzinduzi wa program ya SWAHIBA Mobile mapema hii leo.
"Huduma
hii pia inakuja kutia msistizo wa ahadi yetu ya kuweka mapendekezo ya
wateja wetu kwanza na kuwaongezea uzoefu wa kidigitli Zaidi katika
ukuwaji wa sayansi na technologia. Mkurugenzi aliendelea kueleza “Pia
inathibitisha uamuzi wa benki wa kujenga uwepo wake wa kidigitali na
kukidhi mahitaji ya haraka ya wateja wetu "
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...