Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewapongeza Wajasiriamali wa Tanzania kwa ushiriki wao katika Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST.

Dkt. Mwakyembe ametoa pongezi hizo leo mjini Kampala nchini Uganda katika viwanja vya Mashujaa Kololo alipotembelea kujionea namna tamasha hilo lilivyopokelewa na wadau wake walioiwakilisha Tanzania wakiwemo wajasiriamali toka vikundi mbalimbali, vikundi vya ngoma, vikundi vya sanaa ya maigizo pamoja na baadhi ya wasanii.

Katika tamasha hilo, Dkt. Mwakyembe pia alipata fursa ya kutembelea baadhi ya mabanda ya wajasiriamali hao pamoja na kuongea nao huku akijionea bidhaa mbalimbali zinazouzwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jambo ambalo limemfurahisha sana hususani kwa upande wa watu kutoka Tanzania kwakuwa wamejaza mabanda yao kwa bidhaa kadha wa kadha.

“Tamasha hili linaonyesha utajiri mkubwa wa sanaa, utamaduni pamoja na bidhaa tulizonazo kama nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, na hapa tumekutana kwasababu tunabadilishana mawazo na kuonyeshana bidhaa mbalimbali za nchi zetu”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Aidha, katika ziara hiyo, Dkt. Mwakyembe amewatoa wasiwasi wajasiriamali hao kuhusu suala la upatikanaji wa masoko huku akiwaahidi kuwatafutia fursa ya kuwapeleka wajasiriamali hao pamoja na bidhaa zao Bungeni mjini Dodoma ili ziweze kupata soko kwa urahisi kupitia wabunge.

“Niwatoe wasiwasi wajasiriamali wote wa Tanzania mliohudhuria hapa, nitahakikisha kuwa pindi tunaporudi nyumbani nitatafuta wasaa wa kulishawishi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili nyie mpate nafasi ya kuleta bidhaa zenu katika viwanja vya Bunge ili basi Wabunge wapate kujua haswa vitu vizuri mlivyonavyo nah ii itawasaidia kuviuza kwa urahisi zaidi na kujipatia vipato vyenu”, aliongeza Dkt. Mwakyembe.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliyokuwa ikipigwa na Kikundi cha Sanaa na Utamaduni Tanzania (TaSUBA) katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza mjasiriamali wa Tanzania kuhusu baadhi ya bidhaa zilizopo katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea zawadi ya shati toka kwa mjasiriamali wa Tanzania mara alipotembelea banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye tai nyekundu) akiangalia moja ya ubunifu wa picha iliyochongwa na mjasiriamali wa Tanzania wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...