Na.Thobias Robert- MAELEZO.

Serikali imelipongeza Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) kwa ushirikiano wake na Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika sekta za Kilimo Afya na Maendeleo ya Jamii kwa kutumia wataalam na uzoefu kutoka Japan.

Pongezi hizo zimetolewa Jijini Dar es Salaam leo na Mkurugenzi Msaidizi wa ushirikiano wa kiufundi kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw.Msafiri Marwa alipokuwa akiwaaga vijana wa kijapani waliokuwa wanajitolea katika sekta ya Kilimo na Maendeleo ya jamii hapa nchini.

“Serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na serikali ya Tanzania katika sekta mbalimbali kama vile kuwajengea uwezo Watanzania kupitia ufadhili wa masomo ya elimu ya juu nchini Japan na kuleta watu wa kujitolea katika miradi ya maendeleo hapa nchini,” alieleza Bw. Marwa.

Aidha, Bw.Marwa ambaye alimuwakilisha Naibu Katibu Mkuu Utumishi Bi. Suzani Mlawi aliipongeza Japan kwa kutumia rasilimali watu pamoja na rasilimali fedha kupitia JICA kufadhili utoaji wa huduma za kijamii jambo ambalo ni kipimo cha ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

Amewapongeza vijana wa kijapan kwa kazi nzuri waliyoifanya hapa nchini katika kipindi chote cha miaka miwili ya kuwahudumia watanzania hasa katika sekta ya Kilimo na Afya.

“Kwa niaba ya serikali niwapongeze vijana wote mliokuja hapa nchini kwa kufanya kazi na jamii ya Watanzania, mmefanya kazi kwa jitihada kubwa wakati mwingine katika mazingira magumu, niwahakikishie kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha mazingira ya ushirikiano ili kuendeleza uhusiano ” alifafanua Marwa.
Mkurugenzi Msaidi wa Ushiririkiano wa Kiufundi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Msafiri Marwa akimkabidhi zawadi kijana wa Kijapan aliyemaliza muda wake wa kujitolea hapa nchini Bw. Yusuke Sakakibara.
Mkurugenzi Msaidi wa Ushiririkiano wa Kiufundi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Msafiri Marwa akimkabidhi zawadi kijana wa Kijapan aliyemaliza muda wake wa kujitolea hapa nchini Kyoko Tada katika hafla ya kuwaaga vijana watatu wa kijapan waliomaliza muda wao wa kujitolea hapa nchini iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Raia wa Japan waliokuwa wakijitolea nchini kupitia Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA) wakiwa katika hafla ya kuwaaga baada ya kumaliza muda wao leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Yusuke Sakakibara akiifanya Wilayani Masasi, Shu Sato, Kyoko Tada Mratibu wa vijana wa kujitolea Kutoka JICA nchinI Tanzania Bw. Ichiro Owa mara baada ya hafla kuwaga leo jijini Dar es Salaam.
Picha na: Paschal Dotto – MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...