Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Waandishi wa Habari wakati akitoa taarifa ya mwenendo wa mchakato wa uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na kusema kuwa yoyote atakaye jihusisha na vitendo vya Rushwa asitegemee nafasi ndani ya jumuiya hiyo au chama
 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka, akisisitiza jambo kwa Waandishi wa habari juu ya mwenendo wa Jumuiya hiyo nchini na mafanikio waliyoyapata ndani ya miaka mitatu
 Waandishi wa  Habari walioshiriki mkutano huo wakifuatilia hotuba ya Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shakha Hamdu Shakha.


Ndugu Waandishi wa habari;

Kwa mara nyingine tena tunawakaribisha kwa mikono miwili katika mkutano huu muhimu. Karibuni sana huku nikiwaomba  mjione mko huru na mko nyumbani .

Dhana ya Demokrasia ni jambo muhimu linalohitaji kuheshimiwa na kuenziwa ndani ya Chama na  Jumuiya zake. Kiongozi wa UVCCM mahali popote pale huchaguliwa kwa kufanyika uchaguzi huru na wa  haki unaozingatia Kanuni na Taratibu za Uchaguzi kama zilivyoagizwa na vikao husika bila ya kukiuka, kupuuzwa au kuvunjwa.

Nia ya UVCCM ni kujenga na kudumisha haiba  njema ya kuendelea kuheshimu misingi ya demorasia ya kweli , yenye kuchunga  adabu na kufuata nidhamu, miiko na maadili kwa kila mwanachama anayetaka kutumia haki ya kuchagua au kuchaguliwa.

April Mwaka 2017 Chama Cha Mapinduzi kilianza mchakato wa Uchaguzi ndani ya Chama na Jumuiya zake. Kufuatia mabadiliko ya Kanuni ya UVCCM yaliyofanyika mwezi Machi, 2017 tulianza Uchaguzi katika ngazi za Matawi ambapo hadi leo jumla ya Matawi 23,529  sawa na Asilimia 99.4% kati ya Matawi  23,670 sawa na Asilimia 0.59% yamekamilisha uchaguzi.
Ngazi za   Kata  3,913 sawa na Asilimia 96.59% kati ya Kata 4,051 sawa na asilimia 3.4% zimekamilisha uchaguzi .Kwa upande wa majimbo ya  Zanzibar majimbo 54 sawa na Asilimia 100%, wamekamilisha uchaguzi.  

Ngazi ya Wilaya na Mkoa  mchakato wa uchujaji wa  majina kwa Vijana waliomba nafasi mbali mbali ndani ya Jumuiya yetu , umeanza na  unaendelea vizuri huku jumla ya Vijana 7,606 wamejitokeza kuchuka fomu za kugombea nafasi mbali mbali katka Jumuiya yetu, hali inayoonyesha kumekupo kwa mabadiliko  na msisimko wa kisiasa ukilinganisha na chaguzi zilizopita.

Kwa upande wa ngazi ya Taifa Vijana 350 wamejitokeza kuomba nafasi za uongozi ndani ya UVCCM kama ifuatavyo:-

(i) Nafasi ya Mwenyekiti 113 Walioomba
(ii) Nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa 24 Walioomba
(iii) Nafasi 5 za Wajumbe wa H/Kuu 103 Walioomba
(iv) Nafasi  5 za Wajumbe wa B/Kuu Taifa 81 Walioomba
(v) Nafasi 1 Wawakilishi UWT 14 Walioomba
(vi) Nafasi 1 Wawakilishi Wazazi 15 Walioomba

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...