Na Mwandishi Wetu.
STARTIMES Tanzania kupitia chaneli yake ya Star Swahili kufungua pazia jipya la shindano la kusaka vipaji vya sauti litakalofanyika jijini la Dar es Salaam, Mwanza na Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Meneja Masoko na Mahusiano wa StarTimes Tanzania, Juma Sharobaro amesema  mashindano hayo ni fursa tosha kwa washiriki pamoja na ajira kwa washiki pamoja na washindi hao. 

Amesema kuwa shindano la kusaka vipaji vya sauti litakalofanyika katika maeneo matatu hapa nchini ambayo ni jiji la Dar es Salaam watachukua washindi kumi, jijini Mwanza  watachukua washindi watano na Zanzibar watachukua washindi watano hao wote wataingia fainali itakayohusisha washiriki 20. 

Washindi wa Shindano la kusaka vipaji vya sauti watapata fursa ya kwenda kufanya kazi katika makao makuu ya Startimes yaliyopo jijini Beijing nchini China.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Dkt. Seleman Sewangi amesema kuwa Startimes Tanzania wanasaidia kukuza vipaji vya vijana pamoja na kukuza kiswahili ndani na nje ya Tanzania. 

Amewaasa Startimes kuangalia namna ya wasanii hao kunufaika na kazi zao mara baada ya kumaliza mikataba. Pia alisisitiza kuwepo namna ya kunufaika kati ya nchi mbili ambazo ni Tanzania na Chini katika kazi hizo za sanaa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Dkt. Seleman Sewangi akizungumza kwenye mkutano wa kwanza kati ya Startimes Tanzania pamoja na waandishi wa habari unaohusu shindano la kusaka vipaji vya sauti linaloandaliwa na kampuni ya Startimes kwa kushirikiana na ubalozi wa Chini nchini Tanzania.
Meneja Masoko na Mahusiano wa StarTimes Tanzania, Juma Sharobaro akizungumza na waandishi wa habari na wageni mbalimbali kwenye awamu ya kwanza ya kuandaa shindano la kusaka vipaji vya sauti linaloandaliwa na kampuni ya StarTimes kwa kushirikiana na ubalozi wa Chini nchini Tanzania litakalofanyika Dar Es Salaam, Mwanza na Zanzibar.
Mhadhiri kutoka Taasisi ta Taaluma za Kiswahili(UDSM), George Mrikaria akizungumza kuhusu  chuo hicho kitavyoweza kwenda sambamba na Startimes ili kuweza kuwapata washindi wazuri watakaoitangaza pamoja na kukitangaza kiswahili katika nchi mbalimbali hasa nchini China.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Naitwa Deogratius Mhanga
    Naomba kushiriki katika shindano la Lusaka vipaji vya sauti, kupitia shindano linaloandaliwa na star Swahili nipo Dar es salaam
    0763986115

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...