Mkurugenzi wa shule ya Feza Ibrahim Yunus kushoto na kulia Mwalimu Mkuu wa Feza Boys, Saimon Albert  wakiwa kwenye picha ya pamoja na mshindi wa kwanza hadi watatu wa mashindano hayo. Wa kwanza kushoto ndiye Perfect Ndyetabura  aliyeibuka mshindi wa kwanza kutoka shule ya msingi Hazina  na Hamza Azaeli mwenye miwani aliyeibuka mshindi wa pili naye akitokea shule ya Hazina na watatu anatoka shule ya Feza.

WANAFUNZI wa shule ya Msingi Hazina ya jijini Dar es Salaam, wameibuka washindi kwenye mashindano ya Genius CUP, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Mwanafunzi aliyeshika nafasi ya kwanza  kwenye mashindano hayo ni Hamza Azaeli na Perfect Ndyetabura ambao wote wanatoka shule ya msingi Hazina.

 Mashindano hayo yaliyoshirikisha shule mbalimbali nchini yaliandaliwa na  shule ya Feza na kushirikisha shule kutoka mikoa na kuitaja baadhi ya mikoa iliyoshiriki kuwa ni Tanga, Mwanza, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Pwani, Arusha na Zanzibar.

Mratibu wa mashindano hayo kutoka shule ya Feza, Ashrak Habibu, alisema wanafunzi hao walionyeshana umwamba kwenye masomo ya sayansi na hisabati.

Katika hafla ya kukabidhi vyeti hivyo, iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Kimataifa ya Feza, Salasala jijini Dares Sallam, Mkurugenzi wa shule hiyo, Ibrahim Yunus alisema mashindano hayo ya kimasomo yajulikanayo kama Genius Cup, yaliandaliwa kwa pamoja na shule hizo kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Tume ya Sayansi na Teknolojia.

“Lengo letu ni kuwaandaa wanafunzi ili watakapomaliza masomo yao wawe na taaluma ya kisayansi, hasa kwa kuwa nchi inaelekea katika uchumi wa viwanda, hivyo inahitaji vijana wanasayansi na mashindano haya hufanyika kila mwaka hapa nchini,” alisema mkurugenzi huyo.

 Mbali na kupewa vyeti, wanafunzi watatu waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya Hisabati walitunukiwa kiasi cha fedha 200,000 kwa mshindi wa kwanza (150,000) mshindi wa pili na laki moja kwa mshindi wa tatu.

Akizungumzia  mafanikio ya wanafunzi hao, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,  Patrick Cheche, alisema wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakifanya vyema kwenye mashindano mbalimbali kutokana na maandalizi mazuri wanayoyapata.


 “Walimu wanafanyakazi kwa moyo sana, wazazi wa wanafunzi wamekuwa wakitoa ushirikiano mzuri sana kwa shule na uongozi wa shule unawajali sana walimu, hayo kwa pamoja yamekuwa yakisaidia wanafunzi wetu kufanya vizuri kwenye mashindao mengi,” alisema Mwalimu Patrick

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...