Aliyekuwa kocha msaidizi wa Simba  raia wa Uganda Jackson Mayanja ameamua kuachia ngazi kutokana na matatizo yake binafsi.
Mayanja ambaye bado yuko jijini Dar es Salaam, ameamua kuachana na Simba akidai ana matatizo binafsi na kutapelekea kushindw akutimiza majukumu yake kama kocha msaidizi wa timu hiyo.
Ametanabaisha kuwa matatizo hayo ni ya kifamilia na hataweza kukuyaweja wazi, “Ni matatizo ya kifamilia lakini suala hilo siwezi kulizungumzia kwa sasa,” alisema.
Lakini habari kutoka Simba zimeeleza kuwa sasa wako katika hatua za mwisho kuvunja mkataba wake huku kukiwa na sintofahamu kwa siku za hivi karibuni ndani ya klabu ya Simba ikielezwa kwamba kuna matatizo ya kifedha na ucheleweshwaji wa malipo ya mishahara kwa benchi la ufundi na wachezaji kiujumla.
Taarifa hizo ambazo hazijathibitishwa na uongozi wa Simba haujathibisha taarifa hizo zinazosambazwa kwa sasa kuwa hawajawalipa wachezaji wao mishahara ya miezi mitatu.

x

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...