SABABU
kubwa za wanafunzi wa shule za msingi kutokufanya vizuri darasani
imeelezwa inatokana na uoni hafifi kwa baadhi yao na sio kwamba hawana
akili.
Lakini pia imebainishwa pia kati ya watu 100 kati ya 15
wana kabi liwa na tatizo la macho ambalo limekuwa likiwaathiri kwa asilimia na
kushindwa kufikia malengo yao.
Hayo yalibainishwa juzi na Mratibu wa Huduma za Macho Mkoani
Tanga Dkt Frida Kassiane wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo yalienda
sambamba na upimaji wa macho uliokuwa ukiendeshwa na kampuni ya Noor Optics
inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga.
Alisema hatua hiyo inatokana na baadhi ya wanafunzi
kuumwa macho huku wakiwa hawajitambui kutokana na kutokuwepo kwa utaratibu za
utoaji wa huduma za upimaji machi kwao hususani mashuleni.
“Ukiangalia leo hii baadhi ya wanafunzi utakuwa walikuwa
wakifanya vizuri katika mitihani yao lakini ghafla wanaanza kushuka kiwango na
hili unaweza kukuta linasababishwea na tatizo la macho kama lilivyogundulika
kwa wanafunzi wachache kwenye shule tulizopita “Alisema.
Alisema suala hilo linasababishwa pia na lishe dunia kwa
asilimia kubwa ya watoto wengi ikiwemo kukosa kupata vyakula vilivyokuwa na
virutubisho vinavyoweza kuongeza nguvu na kinga ya macho.
Alisema zoezi hilo ambalo limeanza siku nne zilizopita
limewafikia zaidi ya wanafunzi 1500 katika shule za Msingi,Kwanjeka,Mabokweni
na Nguvumali ambapo baadhi yao walibainika kuna matatizo hayo na kusaidia
matitabu zaidi na kampuni hiyo.
Mwalimu wa shule ya Msingi Nguvumali Jijini Tanga akichukua maelezo ya wanafunzi kabla ya kuanza zoezi la upimaji wa huduma ya macho wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo siku hiyo iliendana na sambamba na upimaji macho ulioendeshwa na Duka la Miwani la Noor Optics kwa kushirikiana na halmashauri ya Jiji hilo kwa wanafunzi wa shule za msingi za mabokweni,kwanjeka na nguvumali,
Mratibu wa Huduma za Macho Mkoa wa Tanga,Dkt Frida Kassiane akiwapima macho mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Nguvumali Jijini Tanga wakati wa siku ya afya ya macho duniani ambapo siku hiyo iliendana na sambamba na upimaji macho ulioendeshwa na Duka la Miwani la Noor Optics kwa kushirikiana na halmashauri ya Jiji hilo kwa wanafunzi wa shule za msingi za mabokweni,kwanjeka na nguvumali,
Amina Nasoro ambaye Mratibu wa Huduma ya Afya ya Macho katika kampuni ya kampuni ya Noor Optics inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga akichukua maeleza ya wanafunzi kabla ya kuwapima.
Amina Nasoro ambaye Mratibu wa Huduma ya Afya ya Macho katika kampuni ya kampuni ya Noor Optics inayojishughulisha na matibabu ya macho na utoaji wa miwani Jijini Tanga akichukua maeleza ya wanafunzi kabla ya kuwapima.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...