Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Mgombea Udiwani wa kata ya Saranga Wilaya ya Ubungo katika uchaguzi mdogo kupitia chama cha Mapinduzi(CCM) ,Haroun Mdoe amechukua fomu rasmi katika ofisi ya Mtendaji wa kata hiyo leo.
Mdoe amechukua fomu hiyo leo mchana akiwa amesindikizwa na wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM ya kata ya Saranga  ambapoiZoezi  hilo la uchukuaji fom lilifanyika katika  ofisi ya afisa mtendaji kata ya saranga  Ndandasi Kijo    ambae ni kaimu Mkurungenzi  wa uchaguzi  katika kata hiyo.
Katika marudio hayo ya uchaguzi vyama mbali mbali  navyo  vimejitokeza kuchuku fomu  hizo ikiwemo   chama cha demokrasia na  maendeleo( chadema),  chama cha wanachi  cuf,  Act wazalendo,  n.k
mara baada ya kuchukua fomu hiyo afisa Mtendaji huyo  Kijo alipiga marufuku  kufanyika kwa kampeni za aina yoyote  kwani  mda wa kampeni bado na hivyo yoyote akibainika  anafanya kampeni shelia kali zitachukuliwa  dhidi ya chama  hicho pamoja na mgombea wake.
 Katibu wa wilaya ya Ubungo, Salum Kali akimkabidhi barua ya uteuzi kwa mgombea Udiwani wa kata ya Saranga kupitia CCM  Mdoe   Katika uchaguzi mdogo unaotaraji kufanyika wilaya ya Ubungo
Mgombea Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mdogo wa Kata ya Saranga, Horoun Mdoe akimkabidhi mtendaji wa kata barua ya uteuzi wake kupitia CCM.
 Mgombea Udiwani Mteule wa Chama Cha Mapinduzi kata ya Saranga  Wilaya ya Ubungo, Haroun Mdoe akisoma kwa umakini barua yake ya uteuzi  kupitia chama chake cha ccm
Baadhi ya viongozi  walio ambatana na mgombea wakati wa kuchukuo fomu wakiwa katika picha ya pamoja
--

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...