Meneja Uhusiano wa Multi Choice Tanzania Johnson Mshana akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani),kuhusiana na shamra shamra mbalimbali katika siku hiyo ya Kampuni ya Multichoice Tanzania kutimiza miaka 20 toka kuanza kutoa huduma katika soko la Tanzania.
Meneja Uendeshaji Baraka Shelukindo akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu Kampuni ya Multichoice Tanzania kutimiza miaka 20 toka kuanza kutoa huduma katika soko la Tanzania. Baraka amesema kuwa katika Kusheherekea maadhimisho ya miaka 20, Multichoice imeandaa maonesho ya siku 2 yatakayofanyika katika ukumbi wa Mlimani City kuanzia siku ya leo Alhamis tarehe 19/10/2017 na kesho Ijumaa tarehe 20/10/2017 kuanzia saa nne asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. "Katika maonesho haya utapata kushuhudia maendeleo ya Teknolojia yetu ya tangu 1997 mpaka sasa na huduma mbali mbali zitolewazo na Multichoice",amesema Baraka.
Mkuu wa Channel ya Africa Bongo Magic Barbara Kambogi akifafanua zaidi kuhusiana na hafla hiyo,alisema kuwa Kutakuwa na mabanda kadhaa likiwemo la Supersport, MNET, Maisha Magic Bongo, Fashion, Banda la watoto na mengine mengi,na kwamba kutakuwepo na Ofa kabambe ndani ya siku 2 za Maonesho, ambapo Mteja atajipatia full set ya DStv kwa sh. 59,000 tu hii ikijumlisha kifurushi cha mwezi mmoja BURE kwa king’amuzi cha HD cha Zappa. Kwa King’amuzi cha Explora Mteja atapata Kwa sh. 240,000 pamoja na kifurushi cha Compact cha mwezi mmoja BURE.
Wanahabari wakisikiliza kwa makini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...