Mgeni Rasmi, Naibu Waziri – Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa akiangalia sehemu ya bidhaa za chakula zilizosindikwa kutoka katika Vikundi vilivyoanzishwa chini ya Ushirika wa Akiba na Mikopo wa TANESCO (TANESCO - SACCOS) katika Viwanja vya Chuo cha Mipango wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kitaifa ya SACCOS inayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Dodoma
Naibu Waziri – Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa akinunua dagaa walioongezwa thamani kutoka kwa kina Mama wa MWACIWOTE SACCOS ya Jijini Mwanza. SACCOS hiyo imeundwa na kina Mama Waalimu wa Shule za Msingi na Sekondari
Mgeni Rasmi, Naibu Waziri – Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa akipa maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Ngome SACCOS Brigedia Jenerali Charo Hussein Yateri namna ambavyo inajiendesha kwa mafanikio makubwa ikiwa na Wanachama zaidi ya 12,500 nchini katika Viwanja vya Chuo cha Mipango wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kitaifa ya SACCOS inayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Dodoma
Mgeni Rasmi, Naibu Waziri – Wizara ya Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa akipa maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa TANESCO SACCOS Bibi Somoe Ismail namna ambavyo inajiendesha kwa mafanikio makubwa ikiwa na Wanachama zaidi ya 5,612 nchini kote katika Viwanja vya Chuo cha Mipango wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kitaifa ya SACCOS inayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Dodoma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...