Na Mwandishi Wetu- Dodoma
Halmashauri
za Temeke na Mbeya zimeonesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa
Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa Watoto waliokinzana na
Sheria ambapo kwa miaka mitano kuanzia 2012 mpaka 2017 jumla ya watoto
1000 wamefikiwa na kupewa msaada wa kisheria na wengine kufutiwa
mashtaka.
Takwimu
hizi zimetolewa mjini Dodoma na Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw.
Rabikira Mushi alipokuwa akifungua kikao cha mwaka cha Tathmini ya Mwaka
ya Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa watoto waliokinzana na
Sheria.
Bw.
Rabikira Mushi ameongeza kuwa katika watoto 1000 waliofikiwa, watoto
416 walipelekwa katika vituo vya marekebisho ambapo wengine wamerudi
shule, kuhitimu mafunzo ya VETA na kurejeshwa katika hali ya heshima na
staha.
“Niseme
Serikali itakuwa inaendelea kutekeleza Mpango huu kwa ubia baina ya
Asasi za Kirai na Halmashauri husika” alisema Bw. Mushi.
Kwa
upande wake Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Mbeya Bi. Bupe Joel
amesema kuwa kwa mkoa wa Mbeya mpango huu ulianza kutekelezwa kuanzia
Novemba, 2014 hadi Oktoba, 2017 kama mpango wa majaribio na umefanikiwa
katika utekelezaji wake kwa kusaidia watoto 185.
“Mpango
huu umesaidia sana kupunguza idadi ya kesi za jinai watoto katika
Mahakama kwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya” alisema Bi Bupe.
Aidha
Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Temeke Bi. Neema Mambosho
amesema kuwa Halmashauri ya Temeke kwa kushirikiana na vituo vya
utekelezaji wa mpango imekuwa ikiangalia njia mbali mbali za kuwasaidia
watoto mara tu wamalizapo muda wao wa kuwa katika mpango wa marekebisho
ya tabia (after care plan).
Ameongeza
kuwa Katika kufanya hivyo Halmashauri imeweza kuwapatia nafasi ya
mafunzo VETA watoto 14 pamoja na kuwasaidia watoto 53 ambao walishaacha
shule kurudi shuleni.
Madhumuni
makubwa ya Mpango wa Marekebisho ya Tabia kwa Watoto waliokinzana na
Sheria ni kuwachepusha watoto kuingia katika mfumo wa mahakama na kwenda
magerezani kutoka na makosa mbalimbali.
Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Watoto Bi Magreth Mussai akifafanua jambo wakati kikao
cha Tathmini ya mwaka ya Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa
watoto waliokinzana na Sheria kilichojumuisha Maafisa Ustawi na
Maendeleo ya Jamii, TAMISEMI, na wadau wa Watoto kilichofanyika katika
ukumbi wa NHIF Mjini Dodoma.
Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi (katikati) akizungumza na wadau wa utekelezaji wa Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa Watoto waliokinzana na Sheria alipokuwa akifungua kikao cha mwaka cha Tathmini ya Mpango huo katika ukumbi wa NHIF Mjini Dodoma.
Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinisa, Wazee na Watoto Bw. Darius Damas akielezea jambo kwa washiriki wa kikao cha mwaka cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa watoto waliokinzana na Sheria kilichofanyika katika ukumbi wa NHIF Mjini Dodoma.
Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Mbeya Bi. Bupe Joel akielezea mafanikio ya utekelezaji wa Mpango wa Kijamii wa Marekebisho ya Tabia kwa watoto waliokinzana na Sheria katika Jiji la Mbeya wakati wa kikao cha mwaka cha tathmini ya mwaka ya Mpango huo kilichofanyika katika ukumbi wa NHIF Mjini Dodoma.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...