Waziri wa Mafuta na Gesi kutoka Serikali ya Oman Dkt. Mohamed Bin Hamed Al–Rumhi akinywa maji toka katika kisima cha maji ya baraka kilichopo katika eneo la ulipojengwa msikiti wa kwanza pwani ya mashariki katika eneo la Kaole wilayani Bagamoyo wakati wa ziara yakutembelea eneo la Bandari ya Bagamoyo iliyopo Mbegani, maeneo ya uwekezaji na historia wilayani Bagamoyo leo. 
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akiwaonyesha eneo la bahari ujumbe kutoka Serikali ya Oman unaoopngozwa na Waziri wa Mafuta na Gesi kutoka Serikali ya Oman Dkt. Mohamed Bin Hamed Al–Rumhi (mwenye miwani mwenyeusi) walipotembelea eneo la Bandari ya Bagamoyo iliyopo Mbegani katika ziara ya kutembelea maeneo ya uwekezaji na historia wilayani Bagamoyo leo. Mwenye vazi la kitenge ni Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stellah Manyanya.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Alhaji Majjid Hemed, Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, Waziri wa Mafuta na Gesi kutoka Serikali ya Oman Dkt. Mohamed Bin Hamed Al–Rumhi Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stellah Manyanya wakitoka katika Bandari ya Bagamoyo wakati wa ziara ya Waziri huyo katika maeneo ya uwekezaji kiuchumi (EPZA), maeneo ya kihistoria la Kaole na eneo itakapojengwa bandari mpya.

Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Utalii wa Oman Bi. Maitha Saif Majid Al- Mahrouqi, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo, Waziri wa Mafuta na Gesi kutoka Serikali ya Oman Dkt. Mohamed Bin Hamed Al–Rumhi, Balozi wa Oman nchini Tanzania Mhe. Ali A. Al Mahruqi na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Alhaj Majjid Hemed wakimsikiliza mhifadhi ya makumbusho ya mali kale ya Kaole walipotembelea eneo hilo leo.
Waziri wa Mafuta na Gesi kutoka Serikali ya Oman Dkt. Mohamed Bin Hamed Al–Rumhi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Tanzania mara baada ya kutembelea eneo itakapojengwa bandari mpya wilayani Bagamoyo leo. Kushoto ni Balozi wa Oman nchini Tanzania Mhe. Ali A. Al Mahruqi, Balozi wa Tanzania nchini Oman Abdallah Kilima, Naibu Waziri wa Utalii wa Oman Bi. Maitha Saif Majid Al- Mahrouqi, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo,Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stellah Manyanya, Waziri wa Uwekezaji wa Oman Salem Bin Nasser Al Ismaily. 
Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...